Na Mwandishi Wetu, Ruvuma. MBUNGE wa Vijana Mkoa wa Ruvuma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga ameendelea kuhamasisha Wananchi katika maeneo mbalimbali mkoani hapa ili waweze kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27 mwaka huu. Baada ya ziara ya mafanikio aliyoifanya wilayani Namtumbo, Mhe. Kapinga amefanya ziara pia wilayani Mbinga kwa kuanza na Vijiji vya Mkako na Kigonsera ambapo amewaasa Wananchi kuchagua Viongozi bora watakaosimamia shughuli za maendeleo katika Mitaa, Vijiji na Vitongoji hapa nchini. "Wananchi mliopo katika Kata ya Kigonsera, Mkako na maeneo yote ya Mbinga ifikapo Novemba 27, 2024 jitokezeni kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa ili mchague Viongozi makini kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), " amesisitiza Kapinga. Amesema kuwa, lazima umakini uwepo katika uchaguzi wa Viongozi kwani ndio watakuwa wasimamizi wakuu wa miradi ya maendeleo kwenye ma...