Skip to main content

Posts

Showing posts from February 9, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia Aridhia Malipo ya Fidia Barabara ya Afrika Mashariki-kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Dr. Samia Suluhu ameridhia malipo ya shilingi Milioni 800.65 kwa wananchi 429 wa Kata ya Mkange wanaopisha ujenzi wa Barabara ya Afrika Mashariki inayojengwa toka Tanga kupita Kata hiyo hadi Makurunge Bagamoyo.  Akizungumza katika mkutano huo na wananchi wa vijiji Vitano vya kata hiyo, Mbunge wa jimbo la Chalinze ambaye pia ni Waziri Wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana,Ajira na wenye Ulemavu Ndugu Ridhiwani Kikwete aliishukuru serikali kwa kuendelea kutatua kero za wananchi na kumshukuru Mh. Rais kwa kuridhia fedha hizi zilipwe ili wananchi wapishe na kupata maendeleo. Akiishukuru serikali, Mbunge ameeleza shukrani zake kwa serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya barabara mbalimbali katika halmashauri hiyo ambazo zinakwenda kuongeza tija kiuchumi kwa wananchi wanaopitiwa na miundombinu hiyo. Pia Mbunge aliishukuru serikali kwa matayarisho ya ujenzi wa barabara toka Mandera hadi Saadan ambayo inakwenda kufungua fursa kiuchumi. Wakizungum...

Mbunge Ghati Chomete amuhakikishia Wasira Kura za Kishindo za Rais Dkt.Samia Uchaguzi Mkuu 2025

Na Shomari Binda-Serengeti MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mara Ghati Chomete amemuhakikishia Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Bara Stephine Wasira kura za kishindo za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwenye uchaguzi mkuu wa 2025. Ghati amemuhakikishia kiongozi huyo kura hizo ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake mkoani Mara mara baada ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo. Amesema kwa namna ambavyo kazi kubwa imefanywa na Rais Samia ikiwa ni pamoja na kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo kura zitakuwa za kutosha. Mbunge huyo amesema mkoa wa Mara katika sekta ya elimu umenufaika ikiwa ni pamoja na kujengwa shule mpya zilizowezesha watoto wa mkoa wa Mara kupata elimu. Amesema licha ya sekta ya elimu upande wa maji,afya na miundombinu miradi mbalimbali imeendelea kutekelezwa mkoa mzima wa Mara. Mbunge huyo amesema mwanamke wa mkoa wa Mara kupitia miradi ya maji na kutuliwa ndoo kichwani watatoa shukrani kwa kumpigia kura za kishindo Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan. " Mheshimi...

Kamati ya Pic yaridhishwa na Utekelezaji Wa Miradi ya Tawa eneo la Makuyuni

📍 Yathibitisha uwepo wa tija ya uwekezaji Na Beatus Maganja - Arusha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) Mhe. Augustine Vuma Holle (Mb) amesema Kamati yake imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya utalii inayofanywa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA katika Hifadhi ya eneo la Makuyuni Wildlife Park iliyopo wilaya ya Monduli Mkoani Arusha. Mhe. Augustine ameyasema hayo leo Februari 9, 2025 wakati Kamati yake ilipotembelea hifadhi hiyo kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na TAWA  katika eneo hilo. "Kamati imefurahishwa na namna ambavyo miradi inaendelea, ikumbukwe kwamba hili eneo mara ya kwanza lilikuwa chini ya mwekezaji Kwa muda mrefu sana, baada ya Serikali kuona kwamba hakuna tija eneo hili kuendelea kukaa Kwa mwekezaji, ikalichukua eneo hili na kukabidhiwa msajili wa hazina lakini baadae msajili wa hazina aliwakabidhi TAWA ili waweze kuliendeleza" amesema Mhe. Augustine  "...

Waziri Kikwete atolea Ufafanuzi Ujenzi wa Barabara

 Waziri wan Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na wenye Ulemavu na Mbunge wa Chalinze Mhe, Ridhiwani Jakaya Kikwete leo Februari 9 2025 ametolea ufafanuzi Miradi miwili ya ujenzi wa Barabara ambazo zipo chini ya TANROADS ikiwa ni pamoja na Barabara inayoanzia Mandera hadi Saadani pamoja na Barabara ya Afrika Mashariki ambayo inatokea masuguru hadi pangani.  Ameyasema hayo alipofanya ziara katika Kata ya Mkange na kuzungumza na Wananchi wa eneo hilo na maeneo jirani. Pia amewahakikishia kuwa wale wote ambao maeneo yao yamepitiwa na Barabara hiyo watalipwa stahiki zao kwa kukamilisha nyaraka muhimu.  Aidha Mhe Ridhiwani amewaasa wananchi kuacha kuzungumza kwa kukisia kwani serikali inatambua zoezi la ulipaji wa fidia kwenye maeneo yanayomilikiwa na wananchi pia amewakabidhi rasmi wataalamu kutoka Tanrods ambao watasimamia zoezi la kulipa fidia wananchi hao . Kwaupande wake Mthamini wa Mkoa wa Pwani Tanrods Bi Maria Iranda ametaja baadhi ya vigezo vya kupata fi...

Dkt. Biteko awaasa Waislamu Kuendelea Kuhifadhi Qur’aan Tukufu

📌  Aipongeza Al- Hikma kwa kukuza Mashindano ya kuhifadhi Qur’aan Tukufu 📌  Mashindano ya Qur’aan Tukufu kufanyika mwezi ujao 📌 Mashindano ya Qur'aan Afrika yawa Mashindano Makubwa Zaidi ya Qur’aan Tukufu Ulimwenguni Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewaasa waislamu nchini kuendelea kumcha Mungu na kutenga muda wa kujifunza na kuisoma Qur’aan Tukufu ambayo itawafunza mambo mema yaliyoelekezwa na Mwenyezi Mungu. Dkt. Biteko amesema hayo leo Februari 9, 2025 jijini Dar es salaam wakati akizindua  Mashindano Makubwa zaidi ya Qur’aan Tukufu Ulimwenguni 2025. “ Nawaomba msivunjike moyo akitokea mwenye tafsiri tofauti nyie msivunjike moyo wala kukatishwa tamaa bali mfanye mashindano haya yawe kinara na kuutangaza uislamu katika ulimwengu,” amesema Dkt. Biteko. Pia amewahimiza kumuomba Mungu ili Qur’aan iwanyanyue na isiwabwage katika shughuli mbalimbali wanazofanya kama kaulimbiu ya mwaka...

Wasira Apiga Marufuku Vyama Vya Upinzani Kuwatumia Vijana Mkoa Wa Mara Kufanya Vurugu Mikoa Mingine

*Amtaka waziri Maliasili na Utalii Kufika haraka Serengeti Na Mwandishi Wetu  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema ni marufuku kwa vyama upinzani kuwatumia vijana kutoka mkoani Mara kama nguvu kazi ya kufanya vurugu katika maeneo mbalimbali. Amesema CCM inamipango mizuri kuhakikisha vijana hao wanatumia nguvu zao kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kujikwamua dhidi ya umasikini. Wasira aliyasema hayo jana, alipokuwa akizindua ofisi ya CCM Kata ya Nyakonga wilayani Tarime, Mkoa wa Mara. 'Nataka niwaambie wananchi wa Tarime CHADEMA wakitaka kufanya fujo mahali popote wanakuja kuchukua vijana Tarime...wanapelekwa kufanya fujo kama majeshi ya kukodi, wakitaka kufanya fujo Mbeya wanakuja, Tarima, wakitaka kufanya fujo sehemu Tarime. "Tunawaambia vijana wa Tarime wana mvua wana jua na Tarima panalimika, kila kitu kinaota tuwasaidie vijana wa Tarime watumie fursa zilizopo...tunawaambia CHADEMA muache kuja kuchukua vijana Tarime, sisi sio...