Na Mwandishi Wetu, Mbeya MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Solomon Itunda, amemhakikishia Usalama wakati wote wa huduma za kiroho atakazofanya Jijini Mbeya, mhubiri wa Kimataifa kutoka nchini Kenya Pastor Ezekiel. Sambamba na kumhakikishi Usalama, DC Itunda alipongeza ujio wa Mhubiri huyo wa Injili wa Kimataifa kutoka nchini Kenya, ambaye atafanya mahubiri yake Jijini Mbeya. Pastor Ezekiel atamwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Uchaguzi Mkuu ujao pamoja na amani ya Taifa, hatua ambayo DC Itunda ameieleza kuwa ni ya baraka kubwa kwa nchi. Akizungumza baada ya kupokea wageni hao, DC Itunda alisema ujio wa mhubiri huyo ni ishara ya upendo na mshikamano wa Kikristo unaovuka mipaka ya mataifa hayo jirani. Aliongeza kuwa maombi kwa Taifa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu ni muhimu kwa ajili ya kudumisha mshikamano na mshikamanifu wa Watanzania wote bila kujali imani zao. Katika hotuba yake, Pastor Ezekiel aliwahimiza waumini na viongozi wa dini kuendelea kusali kwa ajili ya amani...
Marato tv - Sauti ya Jamii