Dar es Salaam Wafungwa zaidi ya 600 waliopo katika Gereza kuu Ukonga kufanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo katika kambi maalumu ya siku sita inayofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Kambi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa JKCI kusogeza huduma za kibingwa za moyo karibu na wananchi huku ikitambua kwamba afya ni haki ya kila binadamu na msingi muhimu wa maendeleo ya mtu na taifa kwa ujumla. Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kambi hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema hii ni mara ya kwanza katika Serikali ya Awamu ya Sita kwa JKCI kufikisha huduma hizo za kibingwa katika mazingira ya gerezani.“Kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ni sehemu muhimu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, badala ya kusubiri wananchi wenye changamoto za moyo kusafiri umbali mrefu kuifuata JKCI, imechukua hatua ya kuwafikia wananchi katika maeneo walipo ikiwemo wafungwa wa g...
Marato tv - Sauti ya Jamii