Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo, amewataka Watanzania kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatikana katika Sekta ya Madini ili kujiongezea kipato na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika Pato la Taifa. Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea mabanda kwenye Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili mkoani Geita, Dkt. Lekashingo amesema: “Sekta ya Madini ni injini muhimu ya uchumi wa taifa letu. Hatuwezi kuiacha mikononi mwa wageni pekee, ni lazima sisi kama Watanzania tujitokeze kwa wingi, tuchangamkie fursa zilizopo kuanzia utafiti, uchimbaji, uchenjuaji hadi kwenye biashara na utoaji wa huduma migodini. Tukifanya hivyo, tutajipatia kipato na kuisaidia nchi kuongeza Pato la Taifa.” Ziara hiyo imehusisha pia viongozi mbalimbali wa Tume ya Madini wakiwemo Makamishna wa Tume, Mhandisi Theonestina Mwasha na Dkt. Theresia Numbi; Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, ...
Marato tv - Sauti ya Jamii