Skip to main content

Posts

Showing posts from July 17, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kituo Cha Uwekezaji Tanzania Kuendesha Semina ya Uwekezaji na Vinavyotolewa na Serikali Mkoani Mara

Na Emmanuel Chibasa. Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evance Alfred Mtambi  anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika semina ya maswala ya uwekezaji na vivutio vinavyotolewa na serikali kwa wawekezaji kupitia kituo cha uwekezaji Tanzania(TIC), Semina iliyoandaliwa na kituo cha uwekezaji Tanzania kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mara inatarajiwa kufanyika siku ya Jumanne 23 Julai,2024 katika ukumbi wa uwekezaji uliopo Musoma mkoani Mara. Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, Mkoa wa Mara una idadi ya watu 2,372,015 kutoka 1,743,830 wa  sense ya mwaka 2012. Mkoa wa huu umebarikiwa fursa nyingi za uchumi na uwekezaji kupitia sekta mbalimbali kutokana na uwepo wa hifadhi ta Taifa ya Serengeti ambayo asilimia 70 inapatikana mkoa wa Mara, Ziwa Victoria ambalo ni Ziwa la tatu kwa ukubwa duniani na visiwa vinavyo patikana pia katika ziwa hili vinatoa fursa kubwa za kijamii, kiuchumi, uvuvi, Utalii na umwagiliziaji. Jamii ya wakazi wa mkoa wa Mara wanajishughulisha na s...

Festo Dugange Awataka Watumishi Sekta ya Afya Kote Nchini Kuzingatia Maadili ya Kazi

Naibu Waiziri  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na na Serikali za Mitaa anayeshughulikia elimu Mhe. Dkt. Festo Dugange, amewataka Watumishi wa Sekta ya Afya kote Nchini kuhakikisha wanazingatia utoaji wa huduma kwa kuzingatia Maadili, Lugha nzuri na Uwajibikaji kutokana na viapo vyao vya ya kazi pindi wawapo kazini. Mhe. Dkt. Dugange ametoa maelekezo hayo Julai 16,2024 katika hafla fupi ya Makabidhianao Majengo ya utoaji Huduma ya Uzazi na Mtoto katika kituo cha Afya Haneti kwa ufadhili wa Shirika la KOICA kupitia Shirika la UNICEF Wilayani Chamwino mkoani Dodoma. “Pamoja na kazi nzuri ambazo watumishi wa Afya wamekuwa wakifanya lakini kuna baadhi ya watumishi wa sekta ya Afya wamekuwa wakitoa huduma bila kuzingztia maadili, lugha nzuri na uwajibikaji kulingana na viapo vyao,  hivyo nawakumbusha watumishi wote wa sekta ya afya nchini kuzingatia maadili katika utoaji wa Huduma.” Aidha Dkt. Dugange amesema Tanzania imeendelea kupiga hatua katika kuongeza miundombinu ya upatikan...

Mbunge Vedastus Mathayo Atembelea Hospitali ya Manispaa ya Musoma Aahidi Kutatua Changamoto ya Vifaa Tiba

Na Shomari Binda-Musoma Mbunge wa jimbo la Musoma mjini Mhe.Vedastus Mathayo ametembelea hospitali ya Manispaa ya Musoma na kukutana na Mganga mMfawidhi ili kujua changamoto za huduma. Mhe.Mathayo ametembelea hospitali hiyo leo julai 17, 2024 na kulidhishwa na upatikanaji wa dawa licha ya changamoto ya upungufu wa baadhi ya vifaa tiba. Akizungumza na Mganga  Mfawidhi wa hospital hiyo Dk.Emanuel Shani, amesema huduma bora za afya ni muhimu kwa wananchi na ndio kilichopelekea kuitembelea hospital hiyo. Amesema amelidhishwa kusikia dawa zinapatikana na wananchi wanapofika wanahudumiwa na kupatiwa dawa kwa wsnaohitaji na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi. Mbunge huyo amesema changamoto alizoambiwa za upungufu wa vifaa tiba hasa kwenye chumba cha wagonjwa wa dharura anakwenda kufanyia kazi kwa kuwasiliana na Wizara ya afya. " Kila ninapotoka bungeni napita kwenye maeneo yanayotoa huduma za jamii jimboni kujua changamoto na kuona namna ya kuzipatia ufumbuzi kabla sijaanza mikutano y...

Mathew Kundo Aagiza Ruwasa Mkoa wa Kagera Kutoa Fedha za Kukamilisha Mradi Uliokwama

Na Angela Sebastian-Bukoba Naibu waziri wa maji Mhandisi Mathew Kundo ameagiza wakala wa maji Vijijini- RUWASA- mkoani Kagera  kuwapatia kiasi cha milioni 100 mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira BUWASA ili wampatie mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa maji wa  Bugashani ili akamilishe mradi huo uliokwama. Mhandisi Kundo ametoa agizo hilo wakati alipotembelea eneo palipojengwa  matenki ya maji ya mradi huo utakaonufaisha wananchi wa kata tano,uliopo kata ya Buhembe na kuzungumza na wananchi na watumishi wa mamlaka zote za maji za mkoa wa Kagera.  Kundo amesema  kuwa Serikali haipo tiyali kuona wananchi wake wakiteseka kwa kukosa huduma ya maji hivyo pesa hiyo inatakiwa kupatiwa mkandarasi haraka  iwezekanavyo ili ifikapo Septemba mwaka huu mradi huo uwe umekamilika ili wananchi waweze kupata huduma ya maji. Kadhalika ameongeza kuwa Serikali haipo tayari kuwavumilia wakandarasi wazembe wanaokwamisha miradi ya maji na kupelekea wananchi kupata adha ya kushi...

Jenerali Jacob Nkunda Akutana na Makamanda Toka China

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda Leo kukutana na ujumbe wa makamanda walioongozana na melivita ya matibabu ya Jeshi la Ukombozi la watu wa China 'Peace Ark' ofisini kwake Upanga jijini Dar Es Salaam na kufanya mazungumzo naye. Katika mazungumzo hayo Kiongozi wa Ujumbe huo  Rear Admiral HongBo Ying  amelishukuru Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa mapokezi makubwa pamoja na ushirikiano walioupata tangu walipowasili hapa nchini tarehe 16 Julai mwaka huu wakiwa na meli vita ya matibabu. Naye Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amesema JWTZ linapoelekea kuadhimisha kilele cha miaka 60 tangu kuanzishwa kwake, linashirikiana na Jeshi la China katika matibabu na mazoezi ya medani. Amewasihi watanzania kujitokeza kwa wingi kwenye tiba ili kupimwa afya zao pamoja na kupata matibabu bila malipo kwani JWTZ limeamua kushirikiana na Jeshi la China ikiwa ni muendelezo wa ushirikiano kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya JWTZ. Matibabu h...