Skip to main content

Posts

Showing posts from November 23, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Solar Freezer Zinavyoweza Kusaidia Kupunguza Upotevu na Kuharibika Kwa Mazao ya Chakula Baada ya Mavuno

Na Emmanuel Chibasa Tanzania  sawa na nchi nyingine zinazoendelea Duniani, inakabiliwa na upotevu mkubwa wa mazao kati ya asilimia 20 hadi 30 ya mazao ya mkulima, hupotea baada ya mavuno kutokana na wakulima kuwa na uelewa mdogo wa uhifadhi na matumizi ya teknolojia nafuu na safi kama vile nishati ya jua kwa ajili ya kuhifadhi mazao. Upotevu wa chakula kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), hutokea kuanzia shambani baada ya mavuno bila kujumuisha mauzo. Upotevu huo unaweza kufanywa na wakulima, katika mchakato wa uandaaji pamoja na usafirishaji kwa ajili ya uuzaji wa chakula na utupwaji, kwa upande mwingine hutokea sokoni baina ya muuzaji na mtumiaji. Wakati hali hii ikitokea kwa wakulima hapa nchini na duniani Kwa chakula kupotea baada ya mavuno au kuharibika na kutupwa inakadiliwa kuwa kuna watu takribani Milioni 820 duniani kote wanakabiliwa na njaa. Shirika la umoja wa mataifa la chakula na kilimo linaeleza kuwa, ni muhimu kuzuia upotevu na utupwa...

Comoro yasaka Ujuzi na Utaalam kutoka TTCL

  Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Huduma za Mtandao nchini Comoro (ANADEN) Bw. Said Mouinou afanya ziara ya kikazi Shirika la Mawasiliano Tanzania-TTCL leo Novemba 23, 2024 kwa lengo la kupata uzoefu wa usimamizi na uendeshaji wa miundombinu ya mawasiliano nchini Tanzania.  Katika ziara hiyo, wageni kutoka ANADEN wameongozana na Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Mhe. Saidi Yakubu pamoja na Viongozi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wakiongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. David Mwankenja Akizungumza wakati akiwakaribisha Wageni hao kutoka nchini Comoro, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania CPA. Moremi Marwa amewashukuru ANADEN kwa kuchagua Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kuwa ya kujifunza na kuonesha nia yakushirikiana katika kiumarisha sekta ya mawasiliano.  “TTCL tuko tayari kushirikiana na ndugu zetu kutoka Comoro ukizingatia TTCL inauzoefu miaka mingi katika sekta ya mawasiliano.

Mtanzania ashika nafasi ya kwanza mbio za kilometa 10 wanawake nchini Uingereza

   Mwanariadha wa Jeshi la Polisi, Konstebo Transfora Mussa amekuwa mshindi wa kwanza wa mbio za kilometa 10 za Fulham upande wa wanawake zilizofanyika nchini Uingereza Novemba 17, 2024, huku akivunja rekodi ya kukimbia muda mfupi zaidi. Transfora ambaye alipewa medali ya dhahabu, amevunja rekodi hiyo kwa kutumia muda wa dakika 31:53 tofauti na rekodi ya mwaka jana, ambapo mwanariadha kutoka nchini Kenya alishinda kwa kutumia muda wa dakika 33:11 katika mashindano hayo.

Wasimamizi wa Vituo vya Kupigia Kura pamoja na Makarani Katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Watakiwa kuwa Waadilifu

 Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura na Wasimamizi Wasaidizi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza Novemba 23, 2024 wameapishwa pamoja na kupatiwa mafunzo kuhusu Zoezi la upigaji kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini Novemba 27, mwaka huu.  Akizungumza wakati wa mafunzo hayo,Msimamizi wa Uchaguzi katika Halmashauri ya Wilaya hiyo Addo Missama amewataka maafisa hao Kuhakikisha wanafuata taratibu zote za uchaguzi siku ya kupiga kura ili Kuwezesha uchaguzi kufanyika kwa Amani na utulivu.  "Jukumu hili tunapaswa kulifanya kwa uadilifu mkubwa,Tuzingatie kanuni, Sheria na taratibu za uchaguzi zinavyosema,Amani siku ya uchaguzi ipo mikononi mwetu,hivyo tuhakikishe tunatenda haki kwa kila mmoja hadi tukamilishe uchaguzi" alisema Missama na kuongeza kuwa "Wasimamizi wa vituo pamoja na Wasimamizi Wasaidizi muhakikishe mnawahi kwenye vituo vya kupigia kura ambavyo mmepangiwa kusimamia siku ya uchaguzi ili kuweka mazingira sawa ya...

Usiku wa Bwana soko na Bi Lulu Mwanza hotel