· *Makusanyo yafika 105%* MKOA wa Lindi unatarajiwa kuwa lango kuu la uchimbaji wa madini kutokana na kuonekana kuwa na aina zaidi ya 10 za madini mbalimbali yanayopatikana kwa wingi ikiwemo madini ya kimkakati kama Kinywe (Graphite) na Nickel. Akizungumza katika mahojiano maalum, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Lindi, Mhandisi Emmanuel Shija amesema utafiti uliofanywa na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) mwaka 2024 kwa kutumia ndege nyuki umebaini uwepo wa kiasi kikubwa cha madini mkakati ya Kinywe katika eneo la Ruangwa katika Mkoa wa Lindi. Aina nyingine ya madini yanayotambuliwa kuwepo ni pamoja na madini yenye asili ya Chuma, kama Nickel, Dhahabu, Shaba, Manganese na Madini ya viwandani ambayo ni Jasi, Chokaa, Chuma na Chumvi. Mhandisi Shija amesema pia Mkoa wa Lindi unazalisha kwa wingi madini ya viwandani ya Gypsum ambayo yanatumika zaidi kwenye viwanda vya saruji na 'gypsum board' vilivyopo ndani ya nchi na nchi jirani. “Mkoa wa...
Marato tv - Sauti ya Jamii