Skip to main content

Posts

Showing posts from October 21, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule Zote za Sekondari na Msingi Jimbo la Mtumba Kupatiwa Kompyuta Mpakato

Mgombea ubunge wa Jimbo la Mtumba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Anthony Mavunde, ameendeleza kampeni zake katika Kata ya Ihumwa kwa kueleza mikakati ya kuboresha sekta ya elimu na kuinua uchumi wa wananchi kupitia uwekezaji katika miundombinu ya kijamii na biashara. Katika mikakati yake ya kuboresha elimu, Mavunde amepanga kutoa kompyuta mpakato (laptop) kwa shule zote za msingi na sekondari katika jimbo hilo, kwa ajili ya shughuli za kuchapisha mitihani na matumizi ya walimu wakuu. Mpango huo unatarajiwa kukamilika kufikia mwezi Januari, na unatajwa kuwa ni  wa kipekee katika historia ya elimu nchini. "Kila Mwalimu Mkuu na Mkuu wa shule ofisini kwake atakuwa na kompyuta mpakato kwa shule zote za jimbo la Mtumba, pamoja na Kompyuta na mashine za kudurufu mitihani zile gharama za mtihani mnazotoa wazazi nitazibeba mimi mbunge wenu" amesema Mavunde Kwa upande wa Mtaa wa Chang’ombe, Mavunde amesema kuwa Shule ya Msingi Jenerali Msuguri, ambayo ni miongoni mwa shule kongwe k...

Dkt.Nchimbi Ndani ya Jimbo la Momba,Songwe Akifanya 'finishing'' Mikutano ya Kampeni

PICHA mbalimbali za Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi alipofanya mkutano wa  katika uwanja wa Tindingoma, kata ya chiteto,Wilaya ya Momba,mkoa wa Songwe  leo Oktoba 20, 2025, katika muendelezo wa mikutano yake ya hadhara ya kampeni za lala salama ya kusaka kura za ushindi wa kishindo za mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29,2025

NSSF Mwanza yapongezwa kwa kuwakutanisha waajiri

Lulu Mbwaga ;Mwanza Mfuko wa Taifa wa Hilifadhi ya Jamii NSSF, Mkoa wa Mwanza umefanya kongamano la waajiri  kwa lengo la kutoa elimu ya mfumo wa utendaji kazi wa  kidijitali unaoitwa NSSF PORTAL ambao utamsaidia muajiri na muajiriwa kuzifikia huduma za NSSF pasipo kufika ofisini.  Akifungua Kongamano hilo Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana,  Mhe. Amina Makilage, amepongeza uongozi wa NSSF Mkoa wa Mwanza, kwa kuandaa  kongamano la waajiri, kwani kumekua na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi, hivyo    changamoto za watumishi zitatatuluwa kutokana na kuwajengea  uelewa wa pamoja kuhusu Sheria na kanuni za mfuko huo. "Hakikisheni mnatekeleza kwa mujibu wa Sheria Kwa  kwa kupelka mafao kila mwezi kwa wakati na kuhakikisha kuwa wafanyakazi wenu wanajiunga na mfuko wa kijamii utakao wasaidia hapo baadae" Alisema Mhe. Makilage.  Kwa Upande wake, Meneja wa mkoa wa Mwanza, Bwana  Emmanuel Kahensa alisema kuwa,  mfumo huo wa kidigital ume...