Skip to main content

Posts

Showing posts from February 26, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali Yapongeza Uwekezaji Wa Nyihita Sunflower Upatikanaji Wa Mafuta ya Kula

  Na Shomari Binda-Rorya  SERIKALI imepongeza uwekezaji uliofanywa na muwekezaji Nyihita Wilfred wa uanzishaji wa kiwanda na mashamba kwaajili ya uzalishaji wa mafuta ya alizeti. Pongezi hizo zimetolewa jana februari 26 na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exauds Kigahe alipotembelea mashamba na kiwanda cha Nyihita Sunflower wilayani Butiama  na Rorya. Akizungumza mara baada ya kutembelea maeneo hayo amesema Tanzania bado ina upungufu wa viwanda vya mafuta ya kula hivyo wawekezaji wakiwemo wa ndani wanapaswa kulindwa. Amesema mkurugenzi Nyihita amefanya jitihada kubwa kwani licha ya kufanya uzalishaji lakini amekuwa msaada wa kwa kuanzisha programu za kuwasaidia wakulima kupitia kiwanda alichoanzisha. Kigahe amesema serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za uwekezaji unaofanyika kuhakikisha viwanda vilivyoanzishwa vinaendelea. Amesema suala la upatikanaji wa mali ghafi kwaajili ya uzalishaji ni muhimu hivyo suala la kilimo cha umwagiliaji ni muhimu. " Nimshukuru na k...

Mkuu Wa Majeshi Ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda Ateta Na Kamati Ya Usalama Ya Mkoa Wa Ruvuma

 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abass ofisini kwake na kufanya mazungumzo na Kamati ya Ulinzi na Usalama Leo tarehe 27 Februari 2025. Katika mazungumzo yao Jenerali Mkunda amempongeza Mkuu wa Mkoa pamoja na Kamati yaUlinzi na Usalama ya Mkoa huo kwa kuhakikisha kuwa hali ya Usalama katika eneo la mpaka wa Tanzania kwa upande wa Mkoa wa Ruvuma liko salama wakati wote. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Kanali Ahmed Abass Ahmed amelishukuru JWTZ kwa namna linavyohakikisha Mkoa wa Ruvuma unakuwa salama wakati wote hali inayosababisha wananchi wa Mkoa huo na maeneo ya jirani kufanya shughuli zao kwa amani na utulivu.Amemhakikishia kuwa uongozi wa Mkoa utaendelea kutoa ushirikiano kwa JWTZ katika mambo yote ambayo utahusishwa. Kwa mujibu wa Msemaji wa JWTZ Kanali Gaudentius Ilonda,Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi yuko mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja na mambo mengine atashiriki Sherehe za Kumbu...

Balozi Nchimbi Awasili Namibia Msiba Wa Sam Nujoma

  Katibu Mkuu wa Chama Cha Balozi Nchimbi Awasili Namibia Msiba Wa Sam Nujoma (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasili nchini Namibia, akiongoza ujumbe wa CCM kwenye mazishi ya aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Namibia na Baba wa Taifa hilo, Dkt. Sam Shafiishuna Nujoma, yatakayofanyika tarehe 1 Machi, 2025. Balozi Dkt. Nchimbi pamoja na msafara wake aliongozana nao, ambao pia yumo Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Abdalla Hamid, aliwasili Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Hosea Kutako, jijini Windhoek, na kupokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Mhe. Mhe. Caesar Waitara, tarehe 26 Februari 2025.  Balozi Nchimbi atashiriki ratiba mbalimbali za utoaji wa heshima za mwisho na kumuaga Dkt. Sam Nujoma, kuanzia tarehe 27 Februari 2025, ambapo Chama Tawala cha Namibia, SWAPO, ambacho ni rafiki wa kihistoria wa CCM, kimeandaa shughuli kwa ajili ya heshima ya mwasisi wake huyo.  Baada ya hapo, Balozi Nchimbi atashiriki ...

Mwenyekiti Wa Ccm Rorya Akiri Kutoa Fedha Kwa Watendaji Wa Ccm Matawi Na Kata Kinyume Na Maelekezo ya Chama

Na Shomari Binda;Mara MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi  ( CCM) Wilaya ya Rorya Ongujo Wakibara amekili kutoa fedha kwa watendaji wa chama hicho kwenye semina iliyofanyika februari 20. Akizungumza na Waandishi wa Habari katika kutoa ufafanuzi kwa kile kilichoandikwa mitandaoni hivi karibuni amesema alitoa fedha kwa mapenzi yake kwa watendaji hao. Amesema siku ya semina hiyo alifika ukumbini jioni semina ikiwa tayari imemalizika na watendaji wakiwa nje ya ukumbi na waliponiona walirudi ndani nami kwenda kuwasalimia Ongujo amesema kwa kuwa tangu achaguliwe hajawahi kukutana na watendaji hao hivyo baada ya kusalimiana aliwawezesha nauli ambayo hakutaja kiasi. Mwenyekiti huyo amesema amekuwa na kawaida ya kuchangia na kutoa nauli Mara kadhaa na kama kuna kosa kufanya hivyo chama kitanipa maelekezo " Mimi na mbunge tumekuwa tukichangia na kutoa fedha katika kusaidia chama sasa kama ni makosa yatatolewa maelekezo na chama mkoa. " Yale yaliyoandikwa mitandaoni ni ya uongo na yana le...

Ally Hapi Aweka Historia Mpwapwa.

*Asema Rais Samia Ametimiza, Aungwe Mkono* Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Ally Hapi, (MNEC)* ameandika historia wilayani Mpwapwa kwa kupokelewa na kufanya mkubwa wa wananchi eneo la Mpwapwa mjini, tukio ambalo halijawahi kufanyika kwa ukubwa huo katika miaka ya karibuni. Hapi amefanya mkutano mkubwa katika Uwanja wa Mnara wa Mashujaa, ambapo wananchi walijitokeza kwa wingi kumsikiliza ikiwa ni sehemu ya ziara yake wilayani humo. Akihutubia umati huo, ameeleza mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na *Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,* akisisitiza kuwa serikali imeendelea kutekeleza miradi mingi ya maendeleo kwa ufanisi mkubwa ikiwemo kujenga shule mpya za msingi 18, sekondari 13,  madarasa mapya ya shule za msingi 280 na madarasa mapya ya sekondari 313. Aidha, mafanikio mengine aliyotaja Hapi ni ujenzi wa vituo vipya vya afya 5, zahanati 10, umeme vijiji 108 kati ya 113 yote yakiwa yamefanyika katika kipindi cha uongozi wa Dr. Samia Suluhu Hassan. Zi...

Wananchi Musoma Wamtuma Naibu Waziri Kigahe Kwa Rais Dkt.Samia Ufunguzi wa Viwanda

Na Shomari Binda-Musoma  WANANCHI katika manispaa ya Musoma wamemtuma Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exauds Kigahe kufikisha salamu zao kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuifungua kwa ufufuaji na ujenzi wa viwanda. Salamu hizo wamezituma kwa Rais kupitia kikao cha wafanyabiashara wa manispaa ya Musoma na Naibu Waziri  huyo kilicjofanyika leo februari 26 kwenye ukumbi wa uwekezaji uliopo ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mara. Wakizungumza kwenye kikao hicho wamesema mji wa Musoma upo chini kiuchumi kutokana na kufa kwa viwanda vilivyokuwepo na kushindwa kuanzishwa kwa viwanda vipya. Afidh Waziri mmoja wa wachangiaji kwenye kikao hicho amesema kama kutafunguliwa kwa viwanda   vilivyokufa na kuanzishwa mji na mkoa wa Mara kiujumla utafunguka. Amesema viwanda vipya vinaweza kuanzishwa kwa kupatikana kwa wawekezaji wageni watakaoshirikiana na wazawa wenye maeneo bila kuwepo kwa vikwazo. " Tunashukuru umetuletea salamu za mheshimiwa Dkt.Samia na sisi tufikishie salamu zetu kwa...

Mwenyekiti Ongujo Akili Kutoa Fedha Kwa Watendaji Wa Ccm Matawi na Kata Rorya

Na Shomari Binda;Mara MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi  ( CCM) Wilaya ya Rorya Ongujo Wakibara amekili kutoa fedha kwa watendaji wa chama hicho kwenye semina iliyofanyika februari 20. Akizungumza na Waandishi wa Habari katika kutoa ufafanuzi kwa kile kilichoandikwa mitandaoni hivi karibuni amesema alitoa fedha kwa mapenzi yake kwa watendaji hao. Amesema siku ya semina hiyo alifika ukumbini jioni semina ikiwa tayari imemalizika na watendaji wakiwa nje ya ukumbi na waliponiona walirudi ndani nami kwenda kuwasalimia Ongujo amesema kwa kuwa tangu achaguliwe hajawahi kukutana na watendaji hao hivyo baada ya kusalimiana aliwawezesha nauli ambayo hakutaja kiasi. Mwenyekiti huyo amesema amekuwa na kawaida ya kuchangia na kutoa nauli Mara kadhaa na kama kuna kosa kufanya hivyo chama kitanipa maelekezo " Mimi na mbunge tumekuwa tukichangia na kutoa fedha katika kusaidia chama sasa kama ni makosa yatatolewa maelekezo na chama mkoa. " Yale yaliyoandikwa mitandaoni ni ya uongo na yana le...

Walimu Semeni Shida Zenu, Msijione Duni - Dkt. Biteko

  📌 Serikali yatumia mabilioni kulipa madeni ya walimu 📌 Asema walimu ni nguzo ya Taifa 📌 Kliniki ya Walimu neema kwa walimu nchini 📌 CWT yapongezwa kwa kushirikiana na Serikali kutatua changamoto za walimu Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka walimu nchini kuwasilisha changamoto zao na Serikali ipo tayari kuzipatia ufumbuzi na imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuboresha maslahi yao na pamoja mazingira bora ya kazi. Dkt. Biteko ameyasema hayo Februari 26, 2025 mkoani Geita wakati aliposhiriki katika ‘Samia Teacher’s Mobile Clinic - Geita’ inayolenga kusikiliza na kutatua kero za walimu Mkoani Geita. “ Walimu semeni shida zenu na wakati wote msijione duni, oneni namna Serikali inavyoweza kutatua changamoto zenu. Nataka niwakumbushe Watanzania kuwa  ninyi ni nguzo ya taifa letu, zoezi hili linamfanya mwalimu mwenyewe kukutana na watoa huduma Serikalini ili kujua nini kitafanyika juu y...

Jela Miaka 30 Kwa Kumlawiti Binti Wa Wa Miaka 10

Na Dawati la Habari Polisi ; Mwanza Mahakama ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza imemhukuma Slyvester Elias (29) Mkazi wa Kijiji cha Nyehunge, Wilayani humo kwenda jela miaka 30  baada ya kukutwa na hatia ya kumlawiti binti wa miaka 10 (jina linahifadhiwa) kwa sababu za kisheria. Hukumu hiyo ya kesi ya Jinai namba 8399/2024 imesomwa  leo Februari 25,2024 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Sengerema, Evod Kisoka mbele ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nyamhanga Tissoro. Awali, Mwendesha Mashtaka aliieleza Mahakama kwamba mshtakiwa alitenda kosa hilo March,18, 2024, katika Kijiji cha Nyehunge wilaya ya Sengerema, mkoa wa Mwanza kinyume na vifungu vya 154(1)(a) pamoja na kifungu cha (2) cha sheria ya kanuni ya Adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022. Mshtakiwa alifikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza tarehe 29.07.2024 na kusomewa shtaka hilo ambapo alikana. Upande wa Jamhuri ulileta mashahidi na shauri lilianza kusikilizwa katika mahakama hiyo  April ,04 2...