📍 Kamati yaridhishwa na Kasi ya ukuaji wa Taasisi hiyo. Na Beatus Maganja, Dodoma Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA Mej. Jen. (Mstaafu) Hamis R. Semfuko akiambatana na Menejimenti ya TAWA leo Januari 10, 2025 amewasilisha taarifa ya utendaji kazi wa TAWA kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Augustine Vuma Holle (Mb) katika kikao kilichofanyika Ofisi za Bunge jijini Dodoma. Akiwasilisha taarifa hiyo Semfuko amesema TAWA imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha inaongeza mapato Serikalini huku akibainisha uwindaji wa kitalii kuwa chanzo kikuu cha mapato ya TAWA ambapo huchangia takribani 70% ya mapato. Semfuko amesema baada ya UVIKO 19 mapato ya TAWA yamekuwa yakiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka Shillingi Billioni 25.75 mwaka 2020/21 hadi shillingi bilioni 55.57 mwaka 2022/23 na kuongeza kuwa mapato hayo yalizidi kuongezeka kufik...
Marato tv - Sauti ya Jamii