Skip to main content

Posts

Showing posts from May 16, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt. Mwigulu Asema Bima ya Afya Kwa Wote Kuondoa Changamoto za Matibabu

_▪️Asema mfumo huo utarahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi_ _▪️Aonya tabia ya wagonjwa kupelekwa kununua dawa nje_ _▪️Asisitiza hospitali kutokuzuia miili ya marehemu kwa madai ya bili_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote utaondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika kupata huduma za matibabu nchini. Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kondoa Mjini katika Uwanja wa Puma mkoani Dodoma ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi. Waziri Mkuu amesema kupitia mfumo huo wananchi hawatalazimika tena kutumia gharama kubwa katika hatua mbalimbali za matibabu ikiwemo kumuona daktari, vipimo pamoja na ununuzi wa dawa. “Kwa kuwa tunakwenda kwenye utaratibu wa Bima ya Afya kwa Wote, baadhi ya haya mambo yaliyokuwa yanawasumbua wananchi yataenda kupata jawabu la kudumu,” amesema. Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kuboresha hudum...

Jumuiya Wazazi Pangani Yawafunda Wanafunzi Funguni Sekondari

NA: MWANDISHI WETU, PANGANI  Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga wamefundwa masuala mbalimbali yahusuyo elimu, maadili, ukatili wa kijinsia na utunzaji mazingira na viongozi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kilele cha Juma la Wazazi ambapo kiwilaya yamefanyika shuleni hapo. Elimu hiyo imetolewa Mei 16, 2026, na viongozi na wajumbe wa Jumuiya hiyo katika kuhakikisha wanafunzi hao wanafanya vizuri katika masomo yao na kuwajenga katika maadili mazuri ili kujenga jamii yenye maadili na maendeleo. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya na Mjumbe wa Kamati ya Siasa, Waziri Mbezi amewasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidii  ili waweze kutimiza ndoto zao za kimaisha kwani elimu ndiyo uwekezaji bora. "Wanafunzi niwasisitize kufanya bidii sana katika kusoma, maisha yamebadikika, zamani maisha yalikuwa rahisi sana hata bila kusoma mtu ungeweza kuishi, lakini sasa hivi maisha yamebadikika, kila kazi inahitaji mtu aliyesoma". Vilev...

Serikali Yapanga Maboresho ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani

_▪︎ Dkt. Mwigulu asema maghala yawafuate wakulima badala ya wakulima kufuata maghala_ _▪︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inapanga kufanya maboresho katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima hususan gharama na usumbufu wa kufuata huduma za maghala yaliyo mbali na maeneo yao ya uzalishaji. Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi. Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mfumo huo na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha mfumo huo unawanufaisha wakulima kama ilivyokusudiwa. “Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ni wananchi wasiyafuate maghala, maghala yawafuate wananchi pale walipo,” amesema. Aidha, Waziri Mkuu amesema ataitisha kikao ...