Dar es Salaam, 06 Oktoba 2025 Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), kupitia Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imepongeza ushirikiano thabiti kati yake na Benki ya Dunia katika kufadhili na kusimamia utekelezaji wa miradi saba ya maendeleo ya miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege katika baadhi ya mikoa nchini. Akizungumza leo tarehe 06 Oktoba 2025 katika kikao cha ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi inayoendelea chini ya programu ya Tanzania Transport Integration Project for Sustainability (TANTIPS), Mkurugenzi wa Miradi ya Maendeleo wa TANROADS, Mhandisi Japherson Nnko, alisema ushirikiano huo ni mfano bora wa namna Tanzania na Benki ya Dunia wanavyotekeleza miradi ya kimkakati kwa pamoja ili kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji kwa kuzingatia athari za mabadiliko ya tabianchi. Mhandisi Nnko alieleza kuwa miradi hiyo saba inafadhiliwa kwa jumla ya Dola za Marekani milioni 550, sawa na shilingi trilioni 1.3 za Kitanzania, ambapo mi...
Marato tv - Sauti ya Jamii