WATANZANIA 669 waliopo Afrika Kusini wanatarajiwa kurejea nchini kwa hiari yao kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha kurejea nyumbani na kuungana na familia zao. Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, James Bwana, ameyasema hayo leo kuwa utekelezaji wa mpango huo utaanza na kundi la kwanza la Watanzania 241 kutoka Durban, Jimbo la KwaZulu-Natal, watakaorejea nchini Agosti 26, 2026 kwa ndege ya Air Tanzania. Kwa mujibu wa Balozi Bwana, Watanzania hao watafanyiwa uhakiki Agosti 25 na 26 kwa kushirikisha Ubalozi wa Tanzania na mamlaka za Afrika Kusini, kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini. Amesema mpango huo umeanza baada ya Watanzania hao kuomba kwa hiari yao msaada wa Serikali ili waweze kurejea Tanzania, baada ya kuishi Afrika Kusini kwa muda mrefu. “Mheshimiwa Rais amewakaribisha tena nyumbani na amenielekeza kama Balozi wake hapa Afrika Kusini kuhakikisha Watanzania walio tayari kurejea...
Marato tv - Sauti ya Jamii