Na Na Angela Sebastian ;Kagera Wananchi wa Kijiji cha Kaitambunzi, Kata ya Isingiro wilayani Kyerwa, wameiomba Serikali kuchunguza utaratibu unaotumiwa na baadhi ya maafisa wa Uhamiaji wakati wa operesheni za usiku za kusaka wahamiaji haramu, wakidai zimekuwa zikisababisha hofu hata kwa raia wasiokuwa na makosa. Kero hiyo iliwasilishwa katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, Khalid Nsekela, ambapo wananchi walisema wanaunga mkono juhudi za Serikali za kudhibiti uhamiaji haramu, lakini wakasisitiza operesheni zifanyike kwa kuzingatia sheria, taratibu na haki za wananchi. Alistidia Mbatina ni mkazi wa kijiji hicho amesema kuwa licha ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kudhibiti uhamiaji haramu, wanahitaji operesheni hizo kufanyika kwa kuzingatia sheria, taratibu na haki za wananchi ili kuepusha taharuki na hofu isiyo ya lazima ambayo inawakabili kwa sasa. "Operesheni zinazofanyika nyakati za usiku wa manane zimekuwa zikitutia hofu,wanakuja watu wanakamat...
Marato tv - Sauti ya Jamii