Skip to main content

Posts

Showing posts from September 29, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Act Wazalendo Yaahidi Kutatua Changamoto Katika Jamii Utapunguza Malalamiko Kata ya Mwisenge

Na Jovina Massano; Musoma MGOMBEA udiwani Kata ya Mwisenge jimbo la Musoma mjini mkoani Mara Alphonce Dismas  Ochieng ameahidi kutatua changamoto zilizopo kwenye Kata ili kupunguza malalamiko kwa wananchi ameyasema hayo Septemba 28,2025 wakati akinadi sera zake mtaa wa Mkinyerero. Alphonce amesema kumekuwepo na malalamiko mengi kwa jamii hii inatokana na kutokutatuliwa kwa changamoto zinazowakabili wananchi. Amesema baadhi ya mitaa ya Kata hiyo inakabiliwa na changamoto za ukosefu wa miundombinu rafiki ya barabara hasa katika mtaa huo wa Mkinyerero. "Endapo nitapata ridhaa ya kuwa diwani nitawaomba wakala wa barabara mijini na vijijini TARURA kuangalia namna wanavyoweza kutatua changamoto ya barabara hapa Mkinyerero", amesema Alphonce.  Aidha amewaambia wakazi hao kuwa wakimchagua atasaidia kuwezesha wahitaji wenye vigezo walengwa watakaohudumiwa na mfuko wa Kaya maskini (TASAF) tofauti na ilivyo sasa. Amesema wazee wengi wanaachwa ambao wana maisha duni na wanawezeshwa wenye...

Wananchi wa Ubungo wameridhika, wapo tayari kuichagua CCM - Chatanda

  Na: Mwandishi Wetu, Ubungo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda amesema wananchi wa Jimbo la Ubungo Jijini Dar es Salaam wamemuhakikishia kuwa Oktoba 29, 2025, watachagua wagombea wote watokanao na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwani wameridhika na utekelezaji wa Ilani Jimboni hapo. Chatanda ameyasema hayo Septemba 29, 2025 , katika mwendelezo wa ushiriki wake katika ziara ya Mgombea mwenza wa Urais kupitia CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi Jijini Dar es Salaam.  "Mimi kama mratibu na wenzangu tulipowatembelea wanzetu wa Ubungo walituagiza wakasema wanataka tuwape nafasi waonane na Dkt. Samia Suluhu Hassan ili wamwambie kuwa watampa kura za ndiyo, nikawaambia subirini anakuja Dkt. Nchimbi, Mgombea mwenza yeye ndiye mtamwonyesha na kumpa hizo salamu ili awafikishie, sasa leo wapo hapa, utawaona na watakuthibitishia kwamba watampa kura za kishindo, kura za mafuriko," amesema Chatanda. Sambamba na hilo, Chatanda amesisitiza kuwa amepata fursa ya kuon...

📌REA yauza majiko 1,500 kwa bei ya ruzuku kwenye maonesho ya Madini Geita* 📌REA yapongezwa kwa kuuza majiko kwa bei ya ruzuku na kutoa elimu ya miradi ya wakala 📍Geita Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita yamehitimishwa rasmi na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambayo yalifunguliwa Septemba 18 na kufikia kilele tarehe 28 Septemba, 2025 Wakala umeshiriki maonesho hayo kwa kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia, kutoa elimu ya miradi inayotekelezwa na wakala wa nishati vijijini pamoja na fursa zinazopatikana kwa wakala kama vile vituo vidogo vya mafuta. Sambamba na hayo Wakala unahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuuza kwa ruzuku mitungi ya gesi ya kilo 6 ambayo inauzwa kwa bei ya 50% ambayo ni kiasi cha shilingi 17,500 ambapo jumla ya mitungi 5,00 imeuzwa kwa ruzuku kwenye maonesho. Pamoja na hayo, Wakala unafadhili uuzwaji wa majiko banifu yanayotumia mkaa mbadala pamoja na mkaa wa kawaida, majiko hayo yameuzwa kwa bei ya ruzuku ya 85% ambayo ni shilingi 6,195 ambapo bei yake ya kawaida ni shilingi 41,300 ambapo majiko banifu 1,000 yatauzwa kwa bei ya ruzuku katika maonesho hayo. Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini 2025 yamefanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili mkoani Geita

 *📌REA yauza majiko 1,500 kwa bei ya ruzuku kwenye maonesho ya Madini Geita* 📌REA yapongezwa kwa kuuza majiko kwa bei ya ruzuku na kutoa elimu ya miradi ya wakala 📍Geita Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita yamehitimishwa rasmi na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ambayo yalifunguliwa Septemba 18 na kufikia kilele tarehe 28 Septemba, 2025 Wakala umeshiriki maonesho hayo kwa kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia, kutoa elimu ya miradi inayotekelezwa na wakala wa nishati vijijini pamoja na fursa zinazopatikana kwa wakala kama vile vituo vidogo vya mafuta. Sambamba na hayo Wakala unahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuuza kwa ruzuku mitungi ya gesi ya kilo 6 ambayo inauzwa kwa bei ya 50% ambayo ni kiasi cha shilingi 17,500 ambapo jumla ya mitungi 5,00 imeuzwa kwa ruzuku kwenye maonesho. Pamoja na hayo, Wakala unafadhili uuzwaji wa majiko banifu yanayotumia mkaa mbadala pamoja na mkaa wa kawaida, majiko hayo ya...
 Na Angela Sebastian;Bukoba SERIKALI ya mkoa wa Kagera imepokea miradi miwili ya kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi (VVU) kupitia tohara kwa wanaume na wavulana (VMMC) na uwekezaji kwa wasichana na wanawake (Dreams) ambayo ilikuwa inafadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali linaloshughulikia Afya ya jamii katika kuzuia VVU,huduma na matibabu (MDH). Akipokea miradi hiyo  kwa niaba Serikali,katibu tawala msaidizi utawala na rasilimali watu Bwahi Biseko mjini Bukoba amesema, miradi hiyo aliyoipokea ilikuwa ikidhaminiwa kupitia mpango wa dharula wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) ambayo kwanza ni mradi wa tohara ambao umefikia  wanaume na wavulana 539,835 katika mkoa wa Kagera. Amesema takwimu hiyo ni  sawa na asilimi 95 ya waliolengwa tangu mwaka 2016 hadi sasa toka mradi huo ulipoanzishwa kwa lengo la kupambana na maambukizi mapya ya VVU ambapo Serikali imejipanga vyema kuiendeleza. "Sasa kama tumekwishaingizwa katika huduma za kawaida inamaana tunata...

Serikali ijayo ya CCM kurasimisha biashara za wafanyabiashara wadogo

Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi ameendelea na mikutano yake kampeni ndani ya jiji la Dar Es Salaam, ambapo akiwa Wilaya ya Ubungo amesema Serikali ijayo ya CCM imedhamiria kwa dhati kurasimisha biashara za Wafanyabiashara wadogo ili wafanye biashara zenye tija Akiwa katika viunga vya EPZA-Mabibo leo Septemba 29, 2025 wilayani Dkt Nchimbi amewahutubia Wananchi huku akinadi Sera na Ilani ya chama hicho ya 2025-2030 ikilenga kuimarisha sanjari na kupeleka maendeleo kwa Wananchi. Aidha baada ya kuhutubia Wananchi, Dkt Nchimbi pia alipata nafasi ya kuwanadi baadhi ya wagombea Ubunge wa mkoa huo akiwemo Mbunge wa jimbo la Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo pamoja na Madiwani.   Dkt.Nchimbi ni Mgombea mwenza wa Dkt Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 wakipeperusha bendera ya Chama  Cha Mapinduzi (CCM), ambapo mkoa wa Dar es Salaam unakuwa wa 15 kufikiwa ...