Skip to main content

Posts

Showing posts from June 27, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WASIRA: NYERERE AMETUACHIA URITHI USIOFUTIKA MILELE

 Na MWANDISHI WETU, Dar es Salaam Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM - Bara) Ndg Stephen Wasira, amewataka Watanzania kuhifadhi na kuishi kulingana na urithi wa Mwalimu Julius Nyerere. Akizungumza katika mahojiano maalumu, na ujumbe kutoka Serikali ya Angola, leo Juni 27, 2026. Wasira amemuelezea Mwalimu Nyerere kuwa kiongozi wa kipekee ambaye aliwaunganisha wananchi, alitawala kwa uadilifu mkubwa, na kuondoka madarakani bila kujilimbikizia mali. Wasira alisema mojawapo ya sifa kuu za Mwalimu Nyerere ni uwezo wake wa kuwahamasisha Watanzania kushiriki kikamilifu katika masuala muhimu ya kitaifa badala ya kuwa watazamaji ukiwemo ulinzi wa taifa lao. “Aliwashirikisha watu wote. Akieleza sababu ya vita, akawaambia ‘vita hii ni yetu sote.’ kila Mtu alipoona kiongozi wake anamweleza wazi hivi ndivyo ilivyotokea, hivi ndivyo tulivyoamua…basi mtu alishiriki moja kwa moja,” alisema Wasira akirejea Vita ya Kagera. Kuhusu urithi halisi wa Nyerere, Wasira alitaja mambo mawili makuu...

MATAIFA 50 KUSHIRIKI MKUTANO MKUBWA WA MADINI NCHINI TANZANIA

 _Rais Samia Suluhu Hassan kufungua mkutano huo mkubwa mwezi Novemba 2026 -▪️Ni Mkutano mkubwa wa Madini na Uwekezaji ▪️Washiriki 2000 kutoka kushiriki mkutano huo ▪️Kauli Mbiu ya Mkutano inalenga kuongeza thamani madini kwa maendelezo ya Viwanda ▪️Serikali na Sekta Binafsi kushirikiana kuandaa mkutano huo ▪️Waziri Mavunde azindua rasmi maandalizi ya mkutano huo 📍 DAR ES SALAAM.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia S. Hassan anatarajiwa kufungua rasmi Mkutano wa Saba wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIC 2026) utakaofanyika Novemba 19 hadi 21, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Akizungumza leo Juni 27, 2026 wakati wa uzinduzi wa TMIC 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imeamua kujenga uchumi wa viwanda unaotokana na madini kwa kuwekeza katika uchakataji na uyeyushaji wa madini badala ya kuendelea kuuza malighafi. Amesema kaulimbiu ya mkutano huo, "Madini Yaliyoongezwa Thamani: Chach...

DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI LA JENGO LA TAALUMA TIA SINGIDA

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya juu kwa kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia ili kuandaa rasilimali watu yenye ujuzi na uwezo wa kuchangia maendeleo ya Taifa. Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipoweka jiwe la msingi la Jengo la Taaluma la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani Singida. Waziri Mkuu amesema ujenzi wa jengo hilo unaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuboresha mazingira ya elimu ya juu na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi. "Leo hii jengo hili la chuo chetu liko Singida. Hii ni hatua kubwa sana. Hongereni bodi, hongereni chuo, hongereni wanafunzi. Tunawatakia kila la heri," amesema. Aidha, amewapongeza wahandisi, washauri na wakandarasi wazawa wanaotekeleza mradi huo akisema ushiriki wao unaonesha uwezo wa Watanzania katika kutekeleza m...

DKT. MWIGULU: HATUTAFANYA MZAHA NA ANAYETAKA KUVURUGA AMANI YA NCHI

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kulinda amani, usalama wa wananchi na rasilimali za Taifa na haitamvumilia mtu yeyote atakayejihusisha na vitendo vinavyohatarisha usalama wa nchi. Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipowasalimia wananchi wa Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo. Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kufuatilia taarifa kuhusu watu wanaodaiwa kupanga au kufadhili vitendo vinavyoweza kuvuruga amani ya nchi na kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vitaendelea kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo. "Hatutafanya mzaha na mtu wa aina hiyo. Tumepewa jukumu la kuilinda nchi yetu na watu wake, na hatutafanya mchezo kwenye jambo hilo." Amesema Serikali haina mgogoro na chama chochote cha siasa kwa kuwa vyama hivyo vinatambuliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kulinda a...