WANANCHI wa jimbo la Ruangwa mkoani Lindi, wamesema zawadi pekee ya kumlipa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo katika jimbo hilo, ni kushinda uchaguzi wa Serikali za mitaa. Wamesema wamejipanga kushinda vitongoji na vijiji vyote tisini vya jimbo hilo katika uchaguzi huo wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu . Akizungumza baada ya mapokezi makubwa na ya aina yake katika viwanja vya madini jimbo la Ruangwa katika siku ya Hamasa maarufu kama HAMASA DAY, ambayo imeshirikisha vijana wa CCM wa kata 22 za jimbo hilo,mbunge wa Ruangwa ambaye pia ni waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa,amesema Rais Samia,ametoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika jimbo hilo. Amesema hivi sasa kata 22 zina shule za Sekondori na huku baadhi zikiwa na shule zaidi ya moja huku Rais Samia akitoa fedha zaidi za...
Marato tv - Sauti ya Jamii