Na MASHAKA MHANDO, Tanga Serikali imetoa maagizo kwa wizara na taasisi za utafiti nchini kuhakikisha zinakamilisha taratibu zote za kimataifa za kupata ithibati, ili dawa zinazotokana na mimea zikishapita maabara na kuzalishwa viwandani ziache kuitwa 'dawa za asili' na badala yake zitambulike kama dawa za kisasa kutoka Tanzania. Maagizo hayo yametolewa leo Augosti 24 na Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, jana wakati akifunga kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi, na Ubunifu yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga kuanzia Agosti 18 hadi 24, mwaka huu. Akifafanua kuhusu dhana hiyo, Dkt. Mwigulu alitolea mfano dawa ya kutibu tezi dume iliyotengenezwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), akieleza kuwa kuendelea kuziita 'dawa za asili' kunawafanya baadhi ya watu kuwa na ukakasi na mashaka nazo, licha ya kuwa zimepitia michakato yote ya kimaabara kama dawa nyingine za kigeni. "Tuendelee kufanya ...
Marato tv - Sauti ya Jamii