Skip to main content

Posts

Showing posts from January 11, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Meya Gumbo aongoza Harambee Ujenzi Wa Madrasa Msikiti wa Mwisenge Manispaa ya Musoma

Na Shomari Binda-Musoma MEYA wa Manispaa ya Musoma na diwani wa Kata ya Makoko Kapteni mstafu Patrick Gumbo ameongoza harambee kukamilisha ujenzi wa madrasa kufundishia watoto kwenye Msikiti wa Mwisenge uliopo Kata ya Kamnyonge. Harambee hiyo ameiongoza leo januari 11 kwenye kisomo cha Maulid kilichofanyika Msikitini hapo na kuhudhuriwa na watu mbalumbali. Akizungumza kabla ya kuendesha harambee hiyo amesema suala la elimu ya dini kwa vijana lina umuhimu mkubwa hasa kupatika eneo sahihi la kuipatia elimu hiyo. Amesema katika madrasa kunafundishwa maadili mema na kumjua Mwisenge hivyo watoto wakiandaliwa kitapatikana kizazi bora. Gumbo amesema kuchangia katika dini kuna faida kubwa kesho mbele za Mungu na jamii isijikite zaidi kuchangia katika dunia. " Nimepata mualiko wa muda mfupi kutoka kwa Shekh Amani na nimekutana na jambo jema naomba tuungane kulikamilisha. " Mimi nipo dini tofauti lakini katika suala la maendeleo na kuwajenga watoto kiimani tutashirikiana kwa pamoja...

Wakuu wa Nchi na Serikali Afrika Waipa Kongole Tanzania Uzalishaji Mazao ya Chakula Afrika

*Rais Museveni asifu bora wa mchele wa Tanzania, asisitiza kushindana kwa ubora WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema viongozi wa nchi za Afrika wameonesha matumaini makubwa na mikakati iliyowekwa na Tanzania katika kuzalisha mazao ya chakula yenye ubora hasa mpunga na mahindi. Mheshimiwa Majaliwa amewahakikishia Wakuu wa Nchi na Serikali Barani Afrika kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha masuala ya utafiti na kushirikisha sekta binafsi, taasisi za umma zinazojishughulisha na kilimo ili kuhakikisha nchi inakuwa tegemeo katika uzalishaji wa chakula barani Afrika. Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Januari 11, 2025) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Umoja wa Afrika wa kupitisha Programu ya Kuendeleza Kilimo Barani Afrika (CAADP 2026 - 2035) uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha Speke Resort, Munyonyo, Kampala nchini Uganda.  Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali imefarijika kusikia baadhi ya viongozi wa nchi za A...

Wakuu wa Nchi na Serikali Afrika Waipa Kongole Tanzania Uzalishaji Mazao ya Chakula Afrika

*Rais Museveni asifu bora wa mchele wa Tanzania, asisitiza kushindana kwa ubora WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema viongozi wa nchi za Afrika wameonesha matumaini makubwa na mikakati iliyowekwa na Tanzania katika kuzalisha mazao ya chakula yenye ubora hasa mpunga na mahindi. Mheshimiwa Majaliwa amewahakikishia Wakuu wa Nchi na Serikali Barani Afrika kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha masuala ya utafiti na kushirikisha sekta binafsi, taasisi za umma zinazojishughulisha na kilimo ili kuhakikisha nchi inakuwa tegemeo katika uzalishaji wa chakula barani Afrika. Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Januari 11, 2025) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Umoja wa Afrika wa kupitisha Programu ya Kuendeleza Kilimo Barani Afrika (CAADP 2026 - 2035) uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha Speke Resort, Munyonyo, Kampala nchini Uganda.  Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali imefarijika kusikia baadhi ya viongozi wa nchi za A...

Serikali itaendelea kuboresha huduma za uhamiaji - Dkt Biteko

*SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA UHAMIAJI - DKT. BITEKO*  *📌 Aweka jiwe la msingi jengo la Uhamiaji na Makaazi ya Askari* *📌 Dkt. Biteko awapongeza uhamiaji kwa kutoa huduma nzuri* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita imekusudia kuendelea kuboresha huduma mbalimbali za kiuchumi na kijamii zikiwemo huduma za uhamiaji nchini ili kuharakisha maendeleo ya watu. Dkt. Biteko amesema hayo leo Januari 11, 2025 baada ya kuweka Jiwe la Msingi katika jengo la Uhamiaji lililopo katika Wilaya ya Micheweni, Pemba ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za Maadhimisho ya Miaka 61 ya Mapinduzi ya Zanzibar yatakayofikia kilele chake Januari 12, 2025. Amesema Wazanzibari na Watanzania wana kila sababu ya kujivunia maendeleo yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ambapo miradi mbalimbali imetekelezwa ikilinganishwa na kipindi kilichopita. “Mtaku...

Waziri Mkuu Majaliwa akitia saini saini mbele ya Rais Museveni katika mkutano wa Wakuu Nchi na Serikali

  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini mbele ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda (kushoto) na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika baada ya kushuhudia Tamasha la Kahawa Afrika (Africa Coffee Festival) lililolenga kuhamasisha uongezaji thamani katika mazao yanayolimwa Afrika likiwemo zao la kahawa. Tukio hilo lilifanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Speke Resort, Munyonyo, Kampala Uganda ambako alimwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Afrika, Januari 11, 2025.

Waziri Mkuu amwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Katika Mkutano wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika Kuhusu Kilimo

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Januari 11, 2025 ameshiriki Mkutano Maalum wa  Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Afrika ambapo alimwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Speke Resort, Munyonyo, Kampala Uganda. Awali Mheshimiwa Majaliwa alishuhudia   Tamasha la Kahawa Afrika (Africa Coffee Festival) lililolenga kuhamasisha  uongezaji  thamani katika mazao yanayolimwa Afrika likiwemo zao la kahawa. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini mbele ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda  (kushoto) na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika baada ya kushuhudia  Tamasha la Kahawa Afrika (Africa Coffee Festival)  lililolenga kuhamasisha  uongezaji  thamani katika mazao yanayolimwa Afrika likiwemo zao la kahawa.  Tukio hilo lilifanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Speke Resort, Munyonyo, Kampala Uganda ambako alimwakilisha Mheshimi...

Iringa yajipanga Kupandisha Ufaulu na Kusimamia Malezi Katika Shule Zote

Mkuu wa wilaya ya Iringa Komred Kheri James amewataka wadau wa elimu wilayani Iringa kujipanga kikamilifu ili kupandisha ufaulu na kusimamia malezi na maadili ya watoto.                                                       Komred Kheri James ameyasema hayo mapema leo katika kikao kazi cha Wakuu wa shule za Msingi na Sekondari kilichokua na lengo la kuweka mikakati bora ya kuanza mwaka wa masomo na kutoa maelekezo ya Serikali katika maandalizi ya ufunguzi wa shule mapema wiki ijayo.        Akizungumza katika kikao hicho Komred Kheri James ameeleza kuwa wilaya ya Iringa imebarikiwa watoto wenye akili, Walimu wenye uwezo na Serikali imeendelea kuboresha mazingira bora ya utoaji wa elimu, hivyo kuna kila sababu ya kupandisha ufaulu wa watoto katika mitihani yote ya ndani na nje.  Aidha kupitia kikao hicho Mheshimiwa Mkuu wa wil...