WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema bado kuna fursa nyingi hapa nchini ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuongeza idadi ya watalii wa ndani na nje. Ametoa kauli hiyo jana usiku (Jumatano, Agosti 21, 2024) wakati akizungumza na mamia ya wadau na washiriki waliohudhuria tukio la USIKU WA UTALII ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za Tamasha la Kizimkazi 2024 lililofanyika kwenye uwanja wa Maendeleo ya Sheria wa Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar. Amesema kwa kutumia fursa za utamaduni, wanyama na utalii wa fukwe Tanzania inaweza kuongeza idadi ya watalii kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na hali ilivyo sasa. “Hapa Kizimkazi tuna samaki aina ya pomboo ambaye ana sifa zote za kuingia kwenye utalii. Tuendelee kuimarisha utalii wa fukwe na tuwatumie pomboo kuchochea utalii kama ambavyo wenzetu wa Cuba wanawatumia.” “Cuba ni nchi ndogo lakini inapokea watalii wengi sana. Wanao walimu wa kuwafundisha samaki hawa kucheza na binadamu, wanafundishwa kucheza muziki. Na sisi Tanznaia tunao pomboo wa k...
Marato tv - Sauti ya Jamii