WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa onyo kwa wasambazaji na wauzaji wa dawa za kulevya kwamba Tanzania siyo mahali pa kufanyia biashara zao. Waziri Mkuu ambaye amefunga maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya Duniani kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema: “Tanzania siyo mahali salama kwa wauzaji, wasafirishaji, walimaji na hata pia watumiaji wa dawa za kulevya. Tanzania tumeiva na sasa tunaenda kukomesha biashara hii.” Ametoa kauli hiyo leo jioni (Alhamisi, Juni 26, 2025) wakati akizungumza na maelfu ya wakazi wa Dodoma wakiwemo wananchi, wadau, viongozi wa Serikali, wa dini na siasa ambao walihudhuria kilele cha maadhimisho hayo kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma. “Makamishna na wakuu wa vyombo vya ulinzi fanyeni kazi, imarisheni ulinzi iwe ni kwenye SGR, vituo vya mabasi, bandari na viwanja vya ndege ili tuweze kuokoa vijana wetu. Dawa hizi zina madhara makubwa kwani zinapoteza uwezo wa mwili na uwezo wa kiakili wa kufikiri ma...
Marato tv - Sauti ya Jamii