Rais Dkt. Samia apiga simu, awataka mabondia Watanzania kuibeba bendera ya Tanzania kwenye tukio hilo_ WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo kuhakikisha inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuwawezesha mabondia kunufaika na vipaji vyao. Ametoa Wito huo jana (Alhamisi, Desemba 26, 2024) wakati wa tukio maalum la pambano la ngumi la ‘Knockout ya Mama’ linalofanyika katika ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam. “Awali michezo hii ilikuwa ni ridhaa, lakini kwasasa tumeweka sheria ambazo zinataka mchezo huu uwe wa kulipwa, ambayo mchezaji akiitwa na kuweka mikataba ni lazima apate maslahi” Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ameitaka Wizara hiyo kwa kushirikiana na wadau wa mchezo wa ngumi kuendelea kuhakikisha wanatoa mafunzo bora kwa makocha na wachezaji. “Hii itawezesha kuwa na uhakika kwamba mabondia wa Kitanzania wanapata ujuzi wa kisasa na wanaendelea kufanya vizuri zaidi”. Katika Hatua Nyingine, Waziri Mkuu ameitaka Wizara hiy...