Na Lubango Mleka, Igunga. WANACHAMA na Mashabiki wa Timu ya Yanga Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora wameadhimisha wiki ya Mwananchi kwa kutembelea wodi ya Watoto katika Hospitali ya wilaya ya Igunga na Gereza la Wilaya ya Igunga na kutoa mahitaji mbalimbali. Kilele hicho kimeanza kwa maandamano ya amani kutokea uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine uliopo Mamlaka ya mji mdogo wa Igunga na kuelekea katika Hospitali ya wilaya ya Igunga na kuwafariji Wazazi na Watoto ambao ni wagonjwa kwa kuwapatia juisi, maji ya kunywa, sabuni za unga na vipande, dawa za miswaki, mafuta pamoja na pampasi. Wamehitimisha maadhimisho hayo kwa kutembelea Gereza kuu wilaya ya Igunga ambapo wametoa kiasi cha sh. 30,000 kwa ajili ya kununua kifurushi cha Azam ili Wafungwa na Mahabusu wapete fursa ya kufuatilia kilele cha wiki ya Mwananchi, aidha wametoa sabuni za unga na vipande, viwembe, maji ya kunywa na mipira miwili kwa ajili ya kufanya mazoezi. Mkaguzi Msaidi I. R. Ntandu kwa niaba ya Mkuu wa gereza la w...
Marato tv - Sauti ya Jamii