Skip to main content

Posts

Showing posts from March 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia Aandikiwa Barua Hii na Kada wa Ccm

 *BARUA YA WAZI KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA* *MH. SAMIA SULUHU HASSAN* YAH. *MAONI YA KUBADILISHA UTARATIBU WA KURUDISHA MAJINA MATATU* Mheshimiwa Mwenyekiti, Husika na kichwa cha barua hapo juu Kutokana na Idadi ya wananchi kuongezeka, Chama chetu pia kimeongeza Idadi ya wanachama wengi wenye sifa na uwezo wa kushika nafasi mbalimbali za Uongozi,  Lakini pia idadi ya wasomi nayo imeongezeka hivyo sasa hivi tuna rasilimali watu kubwa, Idadi hii kubwa inapelekea pia kuwa na wanachama wengi wanaowania nafasi za Uongozi,  Hapo awali wanachama waliokuwa wakiwania nafasi za Uongozi walikuwa wachache na hata wengine walikuwa wakishawishiwa kuombwa kugombea hivyo ilikuwa ni rahisi kuchuja na kupata majina matatu ya wanachama watakaokwenda kupigiwa kura,Lakini sasa hivi hali imebadilika Imefikia hatua mamia na huenda hata maelfu ya wanachama wakajitokeza kuomba ridhaa ya kuwania nafasi za Uongozi hivyo si rahisi kwa majina matatu tu kutosha kumpata mtu sahihi anayestahili kuongoz...

Huu ni Upendo wa Wananchi wa Simiyu Kwa Rais Samia

 

Wizaya ya Maji na DAWASA wakabidhi JKCI hundi ya milioni 20

  Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Maji imeikabidhi Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), hundi la  shilingi milioni 20 kwaajili ya matibabu kwa watoto wenye changamoto mbalimbali  za magonjwa ya moyo. Hundi ya fedha hizo ilikabidhiwa mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu Wizara hiyo,  Mhandisi Mwajuma Waziri  kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dk Angela Muhozya. Akizungumza mara baada ya kukabidhi hundi hiyo, Katibu Mkuu Mwajuma, alisema ziara hiyo ni sehemu ya shamrashamra za wiki ya maji inayofanyika kila mwezi wa tatu kila mwaka  “Sisi tunatambua ukubwa wa tatizo la moyo kwasababu hata sisi hivi karibuni tulimpoteza mfanyakazi mwenzetu ambaye alifariki ghafla mkoani Dodoma kwa hiyo tukisikia mtu anachangamoto ya moyo tunapata hisia kuhusu tatizo hilo,” alisema Alisema Wizara ya Maji imeandaa utaratibu ambapo wafanyakazi wake watakuwa wakifika kwenye taasisi hiyo kwaajili ya kufanya vipimo vya moyo ili watakaobainika kuwa na tatizo watibiwe mapema. Alisema...

Serikali Kuendelea Kushirikiana na Wadau wa Sekta ya Misitu

  Na Happiness Shayo - Njombe  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amesema Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sekta ya Misitu ili kuleta ufanisi na manufaa zaidi katika kuchangia ukuaji wa pato la Taifa (GDP) na kunufaisha wananchi kupitia rasilimali za misitu zilizopo hapa nchini. Ameyasema hayo leo Machi 22, 2025 Mkoani Njombe wakati wa kikao kazi kilichoshirikisha viongozi wa wizara, taasisi na wadau wa sekta ya misitu na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu misitu kwa lengo la kupata ufumbuzi wa kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta hiyo kwa haraka. “Sisi kama Serikali tunajivunia Jukwaa hili kwa kuwa kupitia vikao vyake masuala mengi na ya msingi yamepatiwa ufumbuzi. Kwa masuala ambayo pengine nyie wadau mnaona kuwa bado yana ukakasi, naomba kuwahakikishia kuwa Wizara yangu inaendelea kutafuta ufumbuzi wake” amesema Waziri Chana Waziri Chana amesisitiza kuwa Serikali kupitia ...

Waziri Masauni ahimiza amani na utulivu

  ……Awaandalia futari wadau wa mazingira Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Hamad  Masauni amewahimiza watanzania kutumia nishati safi kupikia kama mkakati bora wa kupambana na mabadiliko ya tabia nchi, uhalibifu wa mazingira na  kuhifadhi viumbe hai. Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa futari aliyoiandaa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC kwa wadau mbalimbali. “Tunapohimiza kuhusu mazingira  hatufanyi haya yote kwa ajili yetu wenyewe, bali kwa vizazi vitakavyokuja baada yetu kwa maana ya watoto na wajukuu zetu. Ni muhimu tuendelee kushirikiana, kufanya kazi pamoja, na kufanya maamuzi ya pamoja ambayo yananufaisha mazingira na watu wanaoyategemea mazingira ambao kwa ujumla ni sisi wenyewe,” alisema. Alisema wadau mbalimbali wanawajibu wa kutengeneza dunia endelevu na yenye maelewano kwa wote huku akisisitiza umuhimu wa kulinda rasilimali zilizopo kwa kuhakikisha zinae...

Ccm Kuja na Ilani ya Kutatua Changamoto za Vijana - Wasira

Na Mwandishi Wetu, Kagera Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema ilani yake ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu, itakuwa na majawabu ya changamoto mbalimbali za vijana ikiwemo namna ya kutatua changamoto ya ajira. Hayo yameelezwa leo Machi 22, 2025 na  Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kemondo, Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuimarisha uhai wa Chama. Amesema kuwa Chama kinafahamu changamoto ambazo vijana wanakumbana nazo na kwamba Ilani ijayo ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030, itakuja na majibu ya shida zao.  “CCM inajua matatizo ya vijana, na imekuwa na mikakati mbalimbali ya kutatua changamoto za vijana. Kwanza CCM imenzishwa na vijana kwani Mwalimu Julius Nyerere alikuwa na miaka 32)  “Lakini hakuna chama cha wazee peke yao labda kiwe chama cha wazee, lakini chama cha siasa lazima kiwe Ccm Kuja na Ilani ya Kutatua Changamoto za Vijana - Wasira v...

Rais Mpya wa Namibia Atangaza Baraza,Mawaziri Kumi Waandamizi Wapigwa Chini

WINDHOEK, Machi 22 Rais wa Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah, ambaye alichukua madaraka siku ya Jana Ijumaa, ametangaza timu yake mpya ya uongozi, ikiwa ni pamoja na uteuzi wa Lucia Witbooi kama Makamu wa rais na Elijah Ngurare kama waziri mkuu. Akitangaza uteuzi huo siku ya Jumamosi huko Windhoek, mji mkuu wa nchi hiyo, Nandi-Ndaitwah, Rais wa tano wa Namibia, pia alianzisha marekebisho makubwa ya wizara na mashirika ya serikali ili kuimarisha ufanisi na kurahisisha shughuli. " "Kama viongozi waliochaguliwa, tuna jukumu kubwa la kuhakikisha kwamba tunaimarisha demokrasia, amani, utulivu na utawala bora nchini, na pia kuharakisha utoaji wa huduma bora za umma kwa Wanamibia wote," Nandi-Ndaitwah alisema katika taarifa yake. Pia alitangaza kupunguza wizara za serikali kutoka 21 hadi 14, na Jumla ya manaibu waziri saba.  Akiangazia mabadiliko muhimu ya kimuundo, Nandi-Ndaitwah alisema kuwa mamlaka ya biashara sasa yatakuwa chini ya Wizara ya Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikian...

Jenerali wa Jeshi la Uganda Ahimiza Ushirikiano wa Majeshi Barani Afrika

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Uganda (UPDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ametoa wito kwa wanajeshi wa Afrika kushughulikia vikwazo vinavyozuia ushirikiano wa kijeshi, akisisitiza jukumu lake muhimu katika kuimarisha utulivu wa kikanda na umoja wa bara.  Akizungumza wakati wa mhadhara kwa maafisa wakuu wa kijeshi katika Chuo cha Kamandi na Wafanyakazi cha Jeshi la Ulinzi la Rwanda (RDF) wilayani Musanze Machi 22 Mwaka huu, Jenerali Kainerugaba alitaja changamoto kama vile migogoro ya kikanda na maendeleo duni, kama vikwazo kwa ushirikiano wa kijeshi. Katika hotuba yake, Jenerali Kainerugaba aliwataka maafisa hao kuwa na mtazamo mpana zaidi, kuvuka mipaka ya kitaifa, na kuweka kipaumbele mifumo kama vile ushirikiano wa kikanda, usalama wa binadamu, na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na washirika wa jadi wa Afrika.  Alisisitiza umuhimu wa hatua za pamoja katika kushughulikia changamoto za pamoja, akibainisha kuwa ushirikiano sio tu unazuia migogoro bali pia unaku...

Raila Odinga ni Baba wa Demokrasia Ukanda wa Afrika-Tundu Lissu

Tumepata heshima ya kukaribishwa na Mh. Raila Amolo Odinga ofisini kwake jijini Nairobi kwa ajili ya mazungumzo juu ya hali ya kisiasa nchini kwetu na harakati za mapambano ya kidemokrasia zinazoongozwa na chama chetu.  Tumepata fursa ya kumweleza RAO juu ya msimamo wetu wa 'No Reform No Election' na kupata uzoefu na ushauri wake. Kama jina lake la utani linavyoashiria, RAO ni 'Baba' wa kweli wa demokrasia katika ukanda wetu wa Afrika. Pamoja na baba yake, Mzee Jaramogi Oginga Odinga, RAO alikuwa mfungwa wa kisiasa wa mara kwa mara wa tawala za Mzee Jomo Kenyatta na Daniel arap Moi.  Licha ya mateso mengi na makubwa akiwa kizuizini katika magereza mbalimbali ya Kenya, 'Baba' hakuwahi kukata tamaa wala kusaliti harakati za kudai demokrasia nchini kwake.  Na Leo tumejua kutoka kwake tulichokuwa hatukijui kabla: alipatiwa passport yake ya kwanza mwaka 1962 (akiwa na umri wa miaka 15!) na Serikali ya Tanganyika baada ya serikali ya kikoloni ya Kenya kumnyima yeye na...

Rais Samia Azindua Sera ya Taifa ya Maji 2002 Toleo la 2025

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Sera ya Taifa ya Maji 2002, Toleo la 2025 katika Ukumbi wa Mlimani City tarehe 22 Machi 2025, Dar es Salaam. Katika hafla hiyo Rais Dkt. Samia ameonyeshwa vifaa mbali mbali vinavyotumika katika utafutaji wa vyanzo na uchimbaji wa visima vya maji.