Skip to main content

Posts

Showing posts from November 8, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Shule ya Sekondari Ruhinda Waiomba REA Kusaidia Kupata Nishati Safi ya Kupikia

  Na Angela Sebastian Karagwe WATUMISHI na wanafunzi wa shule ya sekondari jumuishi ya Ruhinda iliyopo kata ya Nyaishozi wilaya ya Karagwe mkoani Kagera, wameishukuru Serikali kwa kuwafikishia huduma ya Nishati ya umeme kupitia wakala wa Nishati vijijini (REA) pia wameomba kuwaboreshewa miundombinu ya Nishati ya kupikia inayotumiwa na wapishi shuleni hapo kwasasa ni hatari kwa afya zao. Walitoa ombi hilo jana wakati  bodi ya  REA ikiongozwa na mwenyekiti wake balozi meja jenerali mstaafu Jacob Kingu ilipofanya ziara shuleni hapo kwa lengo la kujionea maendeleo ya miradi ya REA vitongojini inayoendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini, ambapo shule hiyo ni miongoni mwa wanufaika. Katika taarifa ya mkuu wa shule hiyo Ambrose Katorogo na shairi kwa niaba ya wanafunzi lililoimbwa na mwanafunzi mwenye uoni hafifu Asifiwe Erasto walisema kuwa kupitia Nishati ya kuni wanayotumia wapishi wa shule hiyo kwa sasa inawaathiri kiafya. Mwalimu Katorogo ameongeza  k...

Uvccm Shanghai Wampongeza Rais Mwinyi kwa Mafanikio

  Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM kutoka Shina la Shanghai, China. Wana-CCM hao walifika kumpongeza Dk. Mwinyi kwa mafanikio makubwa ya miaka minne ya uongozi wake, hususan kwa mchango mkubwa wa kuleta maendeleo ya kiuchumi, kuboresha sekta za kijamii, na kuimarisha diplomasia ya Zanzibar na nchi rafiki ya China. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Westin, Shanghai, ambapo Rais Dk. Mwinyi alipata fursa ya kuzungumza na wana-CCM hao walioongozwa na Ndg. Juma Athumani Sima, Mwenyekiti wa CCM Shina la Shanghai.  Katika salamu hizo, Rais Dk. Mwinyi amewashukuru Wana-CCM wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana, Shina la Shanghai kwa salamu zao za pongezi na kwa kutambua mafanikio ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake.  Kwa upande mwingine, Rais Dk. Hussein Ali Mwinyi a...

Taasisi ya Mama ongea na mwanao yatembelea Hifadhi ya Taifa ya Mikumi

Na Zainab Ally, Mikumi. Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao,inayoundwa na wasanii  mbalimbali wa kuigiza pamoja na nyimbo za Bongo Fleva imevutiwa na vivutio vinavyopatikana Hifadhi ya Taifa Mikumi mkoani Morogoro ambapo wameahidi kuwa mabalozi wa kutangaza hifadhi hiyo hapa nchini. Kiongozi wa ziara hii ya watu zaidi ya 20,Steve Mengele alisema jana tarehe 7/11/2024 kwamba wasanii wote waliotembelea hifadhi hiyo wamevutiwa sana na wanyama wanaopatikana Mikumi wakiwemo ‘Big Four’ ambapo alisema kuwa atahakikisha ziara hiyo inatumika kuitangaza Hifadhi ya Taifa Mikumi. “Tumefurahishwa  sana na utalii wetu tulioufanya katika Hifadhi hii ya Taifa Mikumi,tumeweza kuwaona wanyama mbalimbali wakiwemo ‘Big Four’ ambao ni simba,chui,tembo na nyati,hivyo furaha yetu haitaishia hapa kwani sisi kama wasanii tunaahidi kuitangaza hifadhi hii ya Mikumi”alisema Mengele. Aidha Mengele maarufu kwa jina la Steve Nyerere aliipongeza serikali inayoongozwa na rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedh...

Kamati ya amani ya viongozi wa dini mwanza yataka uchaguzi huru na haki na wenye kuaminika

Wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa mkoani mwanza wametakiwa kutenda haki katika hatua zote za uchaguzi huo ikiwemo uteuzi wa wagombea pamoja na kutangaza matokeo.  Wito huo umetolewa na mwenyekiti mwenza wa kamati ya amani ya viongozi wa dini mkoani humo Sheikh Hassan Kabeke wakati wa kongamano la kuhamasisha ushiriki wa wananchi wa magu Katika uchaguzi wa serikali za mitaa.  "Wasimamizi wa uchaguzi tendeni haki katika uchaguzi huu, muhakikishe mnatangaza washindi halali,hii ni muhimu katika kuwezesha kutamalaki kwa amani na utulivu" alisema Sheikh Kabeke Aidha amewasihi wagombea watakaoshindwa kwenye  uchaguzi wa serikali za mitaa kukubali matokeo ili kuepusha vurugu.  Naye Askofu Dokta Robert Bundala ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya amani ya viongozi wa dini mkoani mwanza amehimiza suala la uzalendo miongoni mwa watanzania Ametaka uzalendo kwa taifa utakuwa na maana ikiwa watu wote waliojiandikisha watajitokeza kuchagua viongozi wanaowataka kat...