Skip to main content

Posts

Showing posts from August 5, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Maendeleo ya Elimu ni Mkombozi wa Taifa Lolote Duniani-Majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa maendeleo katika sekta ya elimu ndio mkombozi na mafanikio ya Taifa lolote duniani. Amesema kwa kutambua hilo, uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan uliamua kuwekeza katika sekta hiyo ili kuhakikisha watoto wa kitanzania wanapata elimu bora katika ngazi zote. Amesema hayo wakati alipozungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya sekondari ya Wasichana ya Lucas Malia iliyopo Ruangwa mkoani Lindi, wakati wa hafla ya kuwapongeza wanafunzi wa kidato cha sita waliofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa iliyofanyika mwaka 2025. “Mliopo shuleni na mnaokuja, tambueni kuwa tuna maeneo muhimu ya kuwaelimisha, mtapata elimu iliyobora na imara itakayowapa maarufa na ujuzi ili muweze kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi” Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita imefanya maboresho ya mitaala kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi yaliyopo duniani ikiwemo mahitaji makubwa ya ajira kwa vijana. “Mabadiliko haya yameifanya mitaa...

Mtasingwa Aibuka Kidedea Kura za Maoni Ccm Jimbo la Bukoba Mjini

  BUKOBA MJINI Mhandisi Johnston Mtasingwa mgombea ubunge wa jimbo la Bukoba Mjini mkoani Kagera kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) ameibuka kidedea katika kura za maoni kwa kupata kura 1,408 huku wenzake wanne walioshiriki uchaguzi huo wakipata kura 1,550. Akitangaza matokeo hayo Katibu wa CCM Wilaya la Bukoba Mjini, Shaban Mdoe ametangaza matokeo hayo ambapo amewataja wengine waliogombea kuwa ni Alex Denis aliyepata kura 804 , Almasoud Kalumuna kura 640 Jamila Hassan kura 66 na Koku Rutha kura 44 Amesema kuwa, wapiga kura waliojiandikisha walikuwa 3,033 waliojitokeza kupiga kura ni 2,978 kura zilizoharibika ni 20 na kura halali zilikuwa ni 2,958.

Mkurugenzi TAMISEMI awataka wananchi kusafisha mitaro ya maji kuzunguka maeneo yao

#Aipongeza TARURA kuendelea kufungua barabara vijijini #Wananchi wa Kimangaro-Mwika Kaskazini wafurahia ushirikiano wa TARURA Dodoma Mkurugenzi wa Idara ya Tawala za Mikoa kutoka OR-TAMISEMI Bi. Beatrice Kimoleta amewataka wananchi kujenga tabia ya kufanya usafi wa mitaro  ya  maji kuzunguka maeneo yao. Bi. Kilemeta ameyasema hayo alipotembelea banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwenye Maonesho ya NaneNane Kitaifa kwenye viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Amesema kwamba wapo baadhi ya wananchi hawasafishi mitaro ya maji kwenye barabara zinazopita kwenye nyumba zao na hivyo maeneo yao kuwa machafu wakati wote. “TARURA endeleeni kutoa elimu kwa wananchi wasafishe mitaro inayopita kwenye nyumba zao,ipo mitaa unakuta kuna barabara nzuri za lami lakini kuna nyasi nyingi na wengine wana magenge mbele ila uchafu wote wanatupa kwenye mitaro hiyo na hawasafishi”. Ameongeza kusema kwamba wananchi wakijenga utamaduni wa kusafisha na kulinda miundombinu ya barabara...