Skip to main content

Posts

Showing posts from April 12, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Aweso: Utendajikazi Uliotukuka Siri ya Rais Samia Kutunukiwa Shahada za Heshima

MWANDISHI WETU - DODOMA Utendajikazi uliotukuka wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa Watanzania na Waafrika kwa ujumla, umetajwa kuwa siri ya kutunukiwa Shahada mbalimbali za Heshima za Udaktari wa Falsafa kutoka vyuo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania. Akizungumzia hayo, Mbunge wa Jimbo la Pangani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amempongeza Rais Dk. Samia kutokana na kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Nasarawa cha nchini Nigeria Aprili 11, 2026, kwa njia ya mtandao. "Rais wetu kipenzi Dk. Samia anafanya kazi kubwa za maendeleo, Watanzania, Waafrika na dunia kwa ujumla wanaziona na kuzitambua kazi zake, ndiyo maana amekuwa akitunukiwa Shahada za Heshima. Uongozi wake uliotukuka umekuwa siri ya heshima hizo anazopata," amesema Aweso. Sanjari na hilo, Aweso amesisitiza kuwa Rais Dk. Samia amejipambanua kwa maneno na kwa vitendo kuwa yeye ni mtekelezaji wa maendeleo ya wananchi ndani na nje ya Tanza...

Waziri wa ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa amwakilisha Waziri Mkuu kuchangia Kanisa la Waadvertista wa Sabato Jimbo Dogo la Mara Kaskazini

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb) tarehe 11 Aprili, 2026, katika jimbo dogo la Mara Kaskazini wilayani Tarime, mkoani Mara amemuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt Mwigulu Lameck Nchemba katika Harambee ya kuchangia ujenzi wa ofisi za mkoa za jimbo la Kanisa la Waadvertista  wa Sabato. Akiwasilisha salamu za Mhe Waziri Mkuu, kwa wananchi na waumini wa kanisa hilo mkoani Mara, Mhe Dkt Rhimo Nyansaho amesema Mheshimiwa Waziri Mkuu anawapongeza Waumini na viongozi wa kanisa hilo kwa hatua ya ujenzi wa Ofisi za mkoa na amepokea kwa heshima mwaliko wa kuwepo kwenye harambee hiyo, lakini kutokana na majukumu ya kitaifa ameshindwa kuwa pamoja nao katika shughuli hiyo muhimu ya kijamii na kiimani. Waziri Mkuu, Mhe Dkt Mwigulu Nchemba katika  salamu zake kwa waumini wa kanisa hao,amewapongeza kwa moyo wa kujitolea walio nao katika kuendeleza kazi ya Mungu.  Akaeleza kuwa taasisi za dini zina mchango mk...

Dkt. Mwigulu: Tunafuatilia Kwa Umakini Suala la Mafuta

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania kuendelea kuwa watulivu na kwamba Serikali inafuatilia kwa karibu na kwa umakini suala la mafuta na kuhakikisha yanaendelea kupatikana nchini ili shughuli za uzalishaji na usafirishaji zisiathirike. Amesema kuwa suala la upatikanaji wa mafuta si jambo la kuamliwa na nchi moja kwa sababu si kila nchi ni muagizaji au mzalishaji wa bidhaa hiyo.”Niwahakikishie Serikali inafuatilia na kila siku kuna vikao tunakaa vya sekta mbalimbali kuweza kuhakikisha  kwamba bidhaa hii haiadimiki na tunashughulika na masuala ya bei ya bidhaa na bei ya huduma.” Waziri Mkuu amesema kwa kutambua umuhimu wa bidhaa hiyo Serikali imelenga kuendelea kuhakikisha inalinda maslahi mapana ya Watanzania kwa sababu haitaki watu washindwe kumudu kupata bidhaa wala kuendesha maisha. Ameyasema hayo leo (Jumapili, Aprili 12, 2026) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mvumi Mision akiwa katika ziara ya...

Waziri Mkuu Akagua Barabara ya Ntyuka - Kikombo

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amekagua ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Ntyuka–Mvumi–Kikombo yenye urefu wa kilomita 76 pamoja na kipande cha barabara ya Chololo–Mapinduzi (Makao Makuu ya TPDF) yenye urefu wa kilomita 5, katika Jimbo la Mvumi, Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma. Mradi huu unaotekelezwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiwa na lengo la kuboresha miundombinu ya usafiri, kuimarisha muunganiko kati ya Wilaya ya Dodoma Mjini na Chamwino, pamoja na kurahisisha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii ikiwemo Hospitali ya Mvumi Mission. Mradi huu unafanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza yenye urefu wa kilomita 25 (ikiwemo Ntyuka–Mvumi–Makulu na Kikombo–Chololo–Mapinduzi) imefikia utekelezaji wa asilimia 80.9, na inatekelezwa na Mkandarasi M/s China Henan International Corporation Company Ltd kwa gharama ya shilingi bilioni 38.199. Awamu ya pili yenye urefu wa kilomita 5...