Skip to main content

Posts

Showing posts from August 29, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Atumia Usafiri wa Treni ya Mwendo Kasi SGR Kutoka Dodoma Hadi Dar es Salaam

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 30, 2024 amesafiri kwa kutumia Usafiri wa treni ya Mwendo Kasi (SGR) kutokea Dodoma kwenda Dar es Salaam ambako atakuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa 12 wa Shirikisho la Watoa Huduma za Afya Afrika Mashariki utakao fanyika katika Kituo  cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

Benki ya NBC Kuchochea Biashara na Agenda ya Uchumi Wa Bluu Zanzibar

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeelezea dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na wafanyabishara wadogo, wa kati na wakubwa kupitia huduma zake mbalimbali za kibenki ili kuchochea ukuaji wa uchumi na mchango wa wadau hao katika kufanikisha agenda ya Uchumi wa Buluu na uwezeshaji wa maendeleo visiwani Zanzibar. Dhamira hiyo imesisitizwa na Meneja wa benki ya NBC tawi la Zanzibar, Bw Abdul Karim Mkila wakati akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bw Theobald Sabi, kwenye hafla fupi ya Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa la Wakuu wa Mashirika na Kampuni  visiwani Zanzibar linalofahamika kama ‘The Tanzanite CEO Roundtable, Zanzibar Chapter’  iliyofanyika visiwani humo jana jioni. Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga aliongoza uzinduzi wa jukwaa hilo, hafla iliyohudhuriwa pia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi, Uchumi na Uwekezaji) Zanzibar, Sharif Ali Sharif. Jukwaa hilo liliwakutanisha pamoja viongozi wa kampuni na mashirika ku...

Waziri Mkuu Awataka Watanzania Kutoa Taarifa za Bidhaa Zisizo Rasmi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania watoe taarifa kwa mamlaka husika pindi wanapokuta kuna bidhaa zisizo rasmi zimeagizwa kutoka nje, zinazalishwa au zinasambazwa nchini. Ametoa wito huo Bungeni leo (Alhamisi, Agosti 29, 2024) wakati akijibu swali la Mbunge wa Hai, Saasisha Mafue kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu. Mbunge huyo alitaka kujua Serikali inatoa kauli gani ili kudhibiti tabia ya vijana kulewa sana nyakati za mchana hali ambayo inasababishwa na uingizaji holela wa pombe kali. “Serikali inao utaratibu wa kutambua uzalishaji na uingizaji wa vileo nchini ambao unadhibitiwa kwa kutoa vibali vya biashara kwa wasambazaji. Vilevile inaendelea kutoa elimu juu ya madhara ya ulevi kupitiliza ili kuwalinda vijana wetu.” Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwahamasisha vijana wajiunge kwenye vikundi ili wafanye shughuli za ujasiriamali. Utaratibu huu umesaidia vijana wetu kupata kipato chao binafsi na f...

Rais Dkt. Samia Amtunuku Nishani ya Miaka 60 Jenerali Jacob Mkunda

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimemtunuku Nishani ya miaka 60, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (CDF) Jenerali Jacob John Mkunda. Mbali na mkuu huyo wa najeshi,wengine waliotunukiwa ni Majenerali, Maafisa pamoja na Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Agosti, 2024. Hafla hiyo pia imehudhuriwa viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo Makamu wa Rais Dkt  Philip Mpango na Rais wa Zanzibar Dkt.Hussein Mwinyi.