MWAKIOJA: UWEKEZAJI WA ZAIDI YA BILIONI 82 KATIKA MAJI WAIPELEKA MKINGA KWENYE LENGO LA ASILIMIA 100
Mbunge wa Jimbo la Mkinga, Mhe. Twaha Said Mwakioja, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya maji wilayani Mkinga, hatua inayoweka msingi wa kumaliza changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi. Akizungumza mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Mhe. Mwakioja amesema wananchi wa Mkinga wana kila sababu ya kuendelea kumpongeza, kumuombea na kumuunga mkono Rais Samia kwa namna ambavyo ameendelea kuelekeza rasilimali nyingi katika miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja. Amesema kwa sasa upatikanaji wa maji safi na salama wilayani Mkinga umefikia asilimia 72.6, huku vijiji 67 kati ya 75 vikipata huduma hiyo. Alibainisha kuwa vijiji vinane vilivyosalia vitaunganishwa na huduma hiyo kupitia miradi ya maji yenye thamani ya takribani shilingi bilioni 47 inayoendelea kutekelezwa. Mbunge huyo amesema, pamoja na miradi hiyo, Serikali imeidhinisha zaidi ya shi...