Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Patrick Adkin Mwalunenge, anaelezwa kuendelea kuweka msukumo mkubwa katika utekelezaji wa agenda ya maendeleo na mageuzi ya uchumi kwa wananchi wa jimbo hilo kupitia mikakati mbalimbali inayolenga kukuza biashara, uwekezaji, ajira na kuboresha miundombinu ya kiuchumi. Katika kipindi kifupi tangu achaguliwe kuongoza jimbo hilo, Mwalunenge ameendelea kushirikiana na wananchi kwa kushuka katika maeneo mbalimbali kusikiliza kero zao, kubaini changamoto zinazowakabili na kuzisimamia ili zipatiwe ufumbuzi. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha maendeleo ya jimbo yanakwenda sambamba na mahitaji halisi ya wananchi. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Ofisi ya Mbunge imejenga mfumo wa kupokea, kuchambua na kufuatilia changamoto za wananchi, huku ikielekeza nguvu katika utekelezaji wa miradi yenye tija kwa uchumi wa Mbeya Mjini na Jiji la Mbeya kwa ujumla. Miongoni mwa maeneo yanayopewa kipaumbele ni kukuza biashara za Mbeya ili ziweze kufikia masoko ya kitaifa na ki...
Marato tv - Sauti ya Jamii