Bi. Winnie Byanyima, mke wa kiongozi wa upinzani wa Uganda aliyekamatwa Dkt. Kizza Besigye, amemshutumu rais wa nchi hiyo mwenye umri wa miaka 81, Yoweri Museveni, kwa kumtayarisha mwanawe kumrithi. Pia alifichua kwamba mumewe, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhaini, alikamatwa kwa kusema kile alichokielezea kama urithi wa kisiasa uliopangwa. "Tunamwona akitupeleka katika mwelekeo hatari wa kumweka mwanawe, [Jenerali Muhoozi Kainerugaba] ambaye tayari amemteua kama mkuu wa jeshi, kuwa rais wetu ajaye. Na ndiyo maana naamini Dkt. Kizza Besigye yuko gerezani, kwa sababu amesema vikali dhidi ya mradi huo. Anaona ni hatari, na nakubaliana naye,". Matamshi yake yanakuja mwaka mmoja baada ya Dkt. Besigye, kiongozi maarufu wa upinzani, kukamatwa kwa utata katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Akizungumzia hali yake, Bi. Byanyima alisema kwamba Dkt. Besigye ametengwa peke yake gerezani. "Haruhusiwi kuzungumza na wafungwa wengine; hawezi kuabudu pamoja na wafungwa wengine; hawezi ...
Marato tv - Sauti ya Jamii