Skip to main content

Posts

Showing posts from July 24, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tarura Iramba Yajenga Daraja la Zege Mto Kinkungu

#Kukamilika kwa daraja hilo kutanufaisha Kata tano Iramba - Singida Kukamilika kwa ujenzi wa daraja la zege katika Mto Kinkungu lenye urefu wa mita 65.6 linalojengwa katika barabara ya Mtoa-Ndago Kata ya Shelui Wilayani Iramba kutanufaisha wananchi wa Kata tano Wilayani humo. Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Kamati ya Ukaguzi ya TARURA ikihitimisha Ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara mkoani Singida. Meneja wa TARURA Mkoa wa Singida Mhandisi Ibrahim Kibasa ameileza Kamati hiyo kuwa Mradi wa ujenzi wa daraja hilo unalenga kuboresha mawasiliano kati ya Kata za Shelui, Mtoa, Ndago, Mtekente na Urughu na kwamba kukamilika kwa mradi huo kutachochea shughuli za maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii katika Kata hizo.  "Licha ya changamoto zilizojitokeza katika hatua za utekelezaji, mradi umefikia hatua ya kuridhisha na matarajio ni kuwa utakamilika ndani ya muda uliopangwa ambao ni  Septemba 15, 2025" alisema Akielezea hali ilivyokuwa hapo awali Mzee Ali Hassan Ju...

Ni Muhimu Kutambulisha Faida Za Soko Huru La Afrika-Ridhiwani

Na Mwandishi Wetu.  Maneno hayo ameyasema Mh. Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu aliposhiriki Uzinduzi wa Mkakati wa Utekelezaji wa Makubaliano ya Mkataba wa Soko Huru la Bara la Afrika , uliofanyika katika Hotel ya Four Season, Dar Es salaam, ulioandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara. Katika hotuba yake , Waziri Kikwete aliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kazi Nzuri wanayoifanya na kuwakumbusha umuhimu wa kutoa elimu ili iwafikie watanzania walio wengi na kuwezesha kuwatambulisha fursa na njia sahihi za kufikia malengo yaliyopangwa na serikali.  Katika maelezo yake alionyesha nia ya kuwasaidia Watanzania kubadili fikra juu ya ufanyaji wa Biashara katika eneo huru la Biashara la Afrika. Katika shughuli hiyo ambayo mgeni wa heshima alikuwa Dkt Selemani Jaffo, Waziri wa Viwanda na Biashara aliwashukuru Mawaziri waliohudhuria na kuwaahidi kuendelea kushirikiana nao kuhakikisha wanafikia malengo kama ilivyoele...

Stamico Yakabidhiwa Leseni Kubwa ya Utafiti na Uchimbaji Madini Adimu Vilima vya Wigu,Morogoro

▪️Ni maelekezo ya Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan ▪️Lengo ni kukuza uwekezaji wa STAMICO kwenye madini mkakati ▪️Waziri Mavunde akabidhi Leseni na kuelekeza uendelezaji wa Leseni kuanza mara moja ▪️Mradi utachochea ukuaji wa Uchumi Morogoro Morogoro Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amekabidhi Leseni ya Utafiti na Uchimbaji Mkubwa wa Madini Adimu na Muhimu ambayo ni ya kimkakati ya Rare Earth Elements (REE) kwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), ikiwa ni hatua muhimu ya kuliwezesha shirika kuingia kwenye shughuli za uchimbaji mkubwa kwa lengo la kuwanufaisha wananchi wote wa Tanzania. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Julai 24, 2025 katika viwanja vya Shule ya Msingi Sesenga kijiji cha Sesenga Kata ya Mgazi Wilaya ya Morogoro, kufuatia uamuzi wa Serikali wa kuirejesha leseni hiyo kutoka kwa kampuni ya Wigu Hill Mining Company Limited baada ya kumalizika kwa shauri la madai kwenye Baraza la Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji(ICSID). Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi waliohud...

Majaliwa aalika wenye viwanda, makampuni, wafanyabiashara kuwekeza nchini

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku mbili nchini Belarus na ametumia ziara hiyo kuwaalika wenye viwanda, makampuni na wafanyabiashara waje kuwekeza nchini. Waziri Mkuu aliwaeleza wakuu wa taasisi aliokutana nao baadhi ya maeneo ya kimkakati kwenye uwekezaji ambayo ni elimu ya juu, afya, kilimo, TEHAMA, uendelezaji viwanda, madini na kukuza utalii.  Alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kukuza uchumi wa Tanzania kwa kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini.  Kwa kuzingatia azma ya Rais Samia, Waziri Mkuu amewahakikishia wenye viwanda na wamiliki wa kampuni zinazotaka kuwekeza nchini, utayari wa Serikali ya Tanzania kushirikiana nazo kwa kuzipatia misaada stahiki zitakapokuja kuwekeza nchini. Amewasihi wenye viwanda vya matreka na mitambo ya kilimo wafungue matawi nchini Tanzania ikiwemo na vituo vya kuhudumuia matrekta (mechanization centres) ili huduma za matrekta ziweze kuwa karibu na wakulima. Vilevile, jana jioni (Jumatano, Julai...

Dkt. Biteko Atoa Wito Vyombo Vya Habari Kuelimisha Jamii Kuhusu Mashujaa

📌Rais Samia mgeni rasmi Maadhimisho ya Mashujaa kesho 📌Atoa wito kwa wananchi kushiriki Maadhimisho ya Mashujaa Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa vyombo vya habari kushirikiana na Serikali katika kuelimisha jamii kuhusu historia ya mashujaa nchini. Dkt. Biteko ametoa wito huo Julai 24, 2025 katika Uwanja na Mnara wa Mashujaa uliopo Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kukagua maadalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa. “ Ninatoa wito kwa wananchi wote kushiriki kwa wingi kwenye tukio hili adhimu. Hii ni siku yetu sote, siku ya kumkumbuka Mtanzania mwenzetu aliyesimama kwa ajili ya Taifa. Vivyo hivyo, nawaomba nyinyi waandishi wa habari, pamoja na vyombo vyenu na pia mitandao ya kijamii mshirikiane na Serikali katika kuelimisha jamii kuhusu historia ya mashujaa wetu, thamani ya mchango wao, na sababu ya sisi kuendelea kuwakumbuka kila mwaka,” amesema Dkt. Biteko. Amezungumzi...