Skip to main content

Posts

Showing posts from September 9, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

RIDHIWANI KIKWETE AMLIWAZA RAIS SAMIA KUFUATIA MSIBA WA MWENZA WAKE

 WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete, ameungana na viongozi wenzake pamoja na wananchi kuhani msiba wa Mzee Hafidh Ameir Hassan, baba na mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja. Katika ziara hiyo, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipata nafasi ya kumfariji Rais Samia na familia yake kufuatia msiba huo mkubwa, huku akimwombea Mwenyezi Mungu ampe nguvu, subira na imani katika kipindi hiki kigumu cha kumpoteza mwenza wake. Mhe. Kikwete amesema anaungana na familia pamoja na Watanzania katika kipindi hiki cha majonzi, akitoa pole kwa Rais Samia na familia yote ya marehemu. “Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un.”

DKT. MWIGULU ATUA ARUSHA, KUFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA HUDUMA ZA AFYA YA MSINGI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo, Septemba 9, 2026, amewasili mkoani Arusha kwa ajili ya kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi. Mkutano huo unafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC)

UKARIMU WA WANATANGA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI TANGA.

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Wadau wa maendeleo mkoani Tanga wameipongeza serikali kwa kuelekeza miradi ya kimkakati katika mkoa huu na kuwataka wananchi kuchangamkia fursa hizi zinazokuja. Wito huo umetolewa na meneja masoko wa Tanga Beach Resort and SPA Firoz Talib alipokuwa akiongea na waandshi wa habari kufuatia uwepo wa miradi mkoani  humo ikiwemo ujio wa Bomba la mafuta ghafi linaloendelea kujengwa huko Chongoleani. Firoz amesema kuwa kutokana na Tanga kusifika katika suala zima la mapishi hivyo basi ni vema wanawake wakachangamkia fursa hiyo kwani imekuja nyumbani na ndio muda wa wao kutamba na kuonesha ujuzi wao kwa wageni wanaokuja. Aidha Firoz pia ameongeza kuwa ujio huo wa miradi Tanga umewapa hamasa kubwa katika maendeleo kwani hapo awali walikuwa na vyumba vya kulala vichache sana lakini kwasasa wamejipanga kuendana na kasi ya maendeleo iliyopo. "Ujio wa Bomba la Mafuta Tanga na miradi mingine imepelekea ongezeko kubwa la wageni kutoka sehemu mbalimbali duniani ...