-ATAKA WAACHIWE WANA CCM CHAGUO LAO Na Shomari Binda-Musoma MBUNGE wa Jimbo la Tarime Vijijini Mwita Waitara amezishukia Kamati za Siasa za Chama cha Mapinduzi ( CCM) za Wilaya ya Musoma mjini na Tarime Vijijini kuacha kuwachagulia mbunge wana CCM wanaomtaka wao. Kauli hiyo ameitoa jana juni 14,2025 kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo kwaajili ya kuwashukuru wananchi kwa kumpa ushirikiano kwa miaka 5 ya uwakilishi wake. Mbele ya wanachama na wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye eneo la soka la kwa saa nane Kata ya Mshikamano amesema yapo mambo ambayo yanafanywa na Kamati hizo za Siasa ambà yo hayapaswi kunyamaziwa. Amesema mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo amefanya kazi nzuri katika utekelezaji wa ilani na anapofanya ziara ya kusoma kamati inakaa pembeni. Waitara amesema hayo mambo sio ya kunyamaziwa kuona watu wanatembea na mgombea wao mfukoni na yale mazuri yaliyofanywa na mbunge wanayabeza Amesema ana...
Marato tv - Sauti ya Jamii