Dk Kellen-Rose Rwakatare achangia milioni 2.2 ujenzi wa madrasa Taqwa na choo cha msikiti Mlimba Na Mwandishi Wetu, Ifakara MWENYEKITI wa Umoja wa Wazazi Mkoa wa Morogoro (UWT), Dk. Kellen-Rose Rwakatare ametoa shilingi milioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa madirisha na milango kwenye Madrasat Taqwa iliyopo msikiti wa Igima uliopo kata ya Mbingu Wilaya ya Mlimba mkoani Morogoro. Akikabidhi msaada huo mwishoni mwa wiki, Dk Rwakatare aliwataka wazazi nchini kujenga tamaduni za kuwa walinzi kwa watoto kwa kuwapeleka kwenye masomo ya dini nyakati za jioni baada ya masomo ya mchana shuleni. Aidha amesema wazaazi hawapaswi kuwaacha watoto wao wakizagaa mitaani na kuwa hatarini kukumbwa na majanga mbalimbali ikiwemo ya ubakaji. Alisema madrasa au sehemu yoyote ya mafunzo ya dini ni sehemu salama kwa mtoto na yenye utulivu ambayo itasaidia mtoto kujifunza dini na maadili na kukua akiwa bora baadae mwenye kuweza kuwa hata kiongozi bora. “Nimewiwa kuja kuchangia madirisha na milango ya madrasa ...
Marato tv - Sauti ya Jamii