WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema kati ya rufaa 16,309 za wagombea wa nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa zilipokelewa, rufaa 5,589 zimekubaliwa. Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Novemba 16, 2024, Waziri Mchengerwa amesema rufaa hizo ni pamoja na zilizowasilishwa baada ya muda wa nyongeza wa siku mbili na uamuzi wake umezingatia dosari ambazo zilisababisha kutoteuliwa kwao awali hazikuwa kubwa zinazoathiri matokeo yaliyokusudiwa na kanuni. Aidha, amesema katika nafasi zinazogombewa vyama 18 vya siasa vimeweka wagombea katika nafasi 30,977 kati ya nafasi 80,430 sawa na asilimia 38.51 huku Chama cha Mapinduzi (CCM) kikiweka wagombea katika nafasi zote. Amesema katika nafasi za mwenyekiti wa kijiji zinazogombewa ni 12,280 ambapo vyama hivyo vimeweka wagombea katika nafasi 6,060 sawa na asilimia 49.35. Pia, amesema nafasi za mwenyekiti wa mtaa zinazogombewa ni...
Marato tv - Sauti ya Jamii