Skip to main content

Posts

Showing posts from June 5, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NCHINI AKUTANA NA MAAFISA WA JESHI LA INDIA

 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa washiriki wa kozi kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa cha India walipotembelea Ofisi za iliyokuwa Makao Makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es Salaam leo tarehe 05 Juni 26. Akizungumza na washiriki wa kozi hiyo, Jenerali Mkunda amesisitiza kuendelea kwa ushirikiano wa kimafunzo kati ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na Jeshi la India ili kuwajengea uwezo kijeshi wanajeshi wa nchi mbili hizi. "Tunashuru kwa kuja kuitembelea Tanzania kwa ziara ya kimafunzo, hii inaonesha jinsi diplomasia ya kijeshi inavyochangia kuongeza weledi na ujuzi kijeshi. Naye, Mkuu wa msafara wa washiriki wa kozi hiyo Rear Admiral…amesema kuwa, kundi la washiriki wa kozi ya NDC India wamejionea jinsi JWTZ linavyoboresha mafunzo yake, na kupongeza maendeleo ya kimafunzo kwa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (Command and Staff Collage) kilichopo Duluti Jijini Arusha. Aidha, Rear Admiral…alipongeza juhudi za Serik...

WAZIRI MKUU ASISITIZA UTOAJI WA HAKI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa haki kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji kwa watumishi wa umma ili kuhakikisha huduma za Serikali zinatolewa kwa ufanisi, kwa wakati na kwa kuzingatia maslahi ya wananchi. Amesema hayo leo Ijumaa, Juni 5, 2026 alipokuwa akizungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa katika Jimbo la Isimani mkoani Iringa katika viwanja vya Isimani tarafani. Dkt. Mwigulu amesema haki za wananchi hazipaswi kucheleweshwa wala kunyimwa kwa sababu yoyote na kusisitiza kuwa kila anayestahili haki yake anapaswa kuipata kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa. “Haki si hisani. Tunataka anayestahili haki apewe haki yake. Serikali haitavumilia vitendo vya kupora au kuchelewesha haki za wananchi kwa sababu yoyote ile,” amesema. Aidha, Waziri Mkuu amesema watumishi wa umma wanapaswa kutambua kuwa nafasi walizonazo ni dhamana ya kuwatumikia wananchi na kwamba huduma zinazoweza kutolewa kwa siku hiy...

TTB YALENGA KUVUTIA WATALII 134,000 KUTOKA URUSI KILA MWAKA

  Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg, Urusi  BODI ya Utalii Tanzania (TTB) inajipanga kumega keki ya utalii inayotengenezwa na Urusi kwa lengo la kulipatia taifa zaidi ya dola za Marekani 500 kwa mwaka. Zaidi ya wananchi milioni 13.4 wa Urusi hutalii sehemu mbalimbali duniani na kutokana na kuwa watumiaji wazuri wa vipato vyao, Tanzania ikipata angalau asilimia 1 ya watu hao ambacho ni sawa na watu 134,000 ambao wataingiza dola milioni 500. Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la Petersburg (SPIEF’26) linaloendelea mjini hapa. Mafuru alisema katika mikakati hiyo wanataka katika miaka 10 ijayo kufikisha watalii mara mbili ya hao na hivyo kuliingizia pato taifa la dola za Marekani bilioni moja. Akiwa katika banda la Tanzania katika jukwaa hilo alisema anafurahi kwa Rais Samia kuendelea kuelekeza maono kwa vitendo katika kusaka wawekezaji. Pia kufungua fursa za Watanzania kwa ziara zinazojumuisha watendaji wakuu wa maen...

RAIS SAMIA AINADI TANZANIA KATIKA KONGAMANO KUBWA LA LA KIMATAIFA NCHINI URUSI

 Na Beda Msimbe, TBN, St Petersburg       Rais Samia Suluhu Hassan leo anahitimisha ziara yake nchini Urusi kwa kushiriki katika kongamano la kibiashara kati ya Tanzania na Urusi sanjari na Jukwaa la Kimataifa la Biashara la St Petersburg.         Katika jukwaa hilo Rais Samia anatarajiwa kuinadi Tanzania katika sekta za uwekezaji na biashara.              Ziara ya Rais Samia imekuwa na mafanikio makubwa hasa hakikisho la ushiriano wa karibu na Urusi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ya uendelezaji wa rasilimaliwatu na ukuzaji wa teknolojia.   Ziara hiyo katika taifa lenye nguvu kubwa kiteknolojia, uchakataji na uzalishaji kwenye kilimo au viwandani imekuja wakati Tanzania inajiandaa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kulifanya taifa kuwa na pato la dola trilioni moja kwa mwaka.                   Kwa sasa serikali ime...

SERIKALI YAZINDUA KITUO CHA OPERESHENI NA MAWASILIANO YA DHARURA MWANZA

 Na, mwandishi wetu – Mwanza SERIKALI imezindua rasmi Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa wa Mwanza, hatua inayolenga kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa na majanga katika mkoa huo. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo leo tarehe 05 Juni, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, amesema kituo hicho ni nyenzo muhimu katika kufuatilia na kudhibiti matukio ya dharura kwa ufanisi zaidi.  Amesema kupitia kituo hicho, mkoa unaweza kufuatilia matukio ya dharura kwa karibu, kukusanya na kuchambua taarifa kwa wakati pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali wa usimamizi wa maafa. “Kupitia kituo hiki, taarifa muhimu zinafika kwa mamlaka husika kwa haraka ili kuwezesha maamuzi stahiki kufanyika kwa wakati,” anasema Mhe.Mtanda. Ameongeza kuwa kituo hicho kinaunganishwa moja kwa moja na Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, hatua inayorahisisha mtiririko wa taarifa na kuimarisha uratibu wa shughuli za kukab...

NAIBU WAZIRI MWINJUMA ARIDHISHWA NA UFUNGAJI VITI MKWAKWANI

 Serikali itaendelea kuboresha viwanja mbalimbali vya michezo nchini ili viweze kutumika katika michuano ya kimataifa hata baada ya Mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027). Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, mara baada ya kutembelea na kukagua usimikaji wa Viti katika Uwanja wa CCM Mkwakwani, jijini Tanga leo Juni 5, 2026. Mhe. Mwinjuma ameupongeza Uongozi wa uwanja huo chini ya Meneja Nassoro Makau, kwa kufanya ubunifu mkubwa wa kuvipanga vizuri viti kwa rangi, ikiwa ni viti vilivyotolewa na Serikali katika uwanja wa Benjamin Mkapa, hatua inayoupendezesha uwanja huo wa kihistoria. Amesema, uboreshaji wa viwanja vya michezo nchini ni sehemu ya maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye Serikali yake ya Awamu ya Sita imewekeza kwa kiwango cha hali ya juu katika ukarabati wa viwanja kama Uhuru na Mkapa, pamoja na ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa Arusha. "Zoezi la usimikaji wa viti hapa Mkwakw...

TANZANIA NA URUSI KUSHIRIKIANA KATIKA KUENDELEZA UTAFITI WA MADINI*

▪️Ni ushirikiano baina ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania(GST) na Chuo Kikuu cha Urusi ▪️Rais Samia afungua fursa zaidi kwa wawekezaji wa madini kutoka Urusi ▪️Madini ya Bauxite yapewa kipaumbele kwenye utafiti *Moscow, Urusi 🇷🇺 * Akishiriki ziara rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Urusi, leo tarehe 05 Juni, 2026 Jijini Moscow, Waziri wa Madini, *Mh. Anthony Peter Mavunde (Mb)* amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Serikali ya Urusi kwenye sekta ya madini ukiongozwa na Naibu Waziri wa Maliasili(Madini) na Mazingira wa Shirikisho la Urusi, *Mh. Tetenkin Dmitry Dmitrievich*. Katika mazungumzo hayo, Waziri Mavunde alieleza namna sekta ya madini inavyozidi kukua na kuonesha fursa mbalimbali zilizopo kwa wawekezaji nchini ikiwemo katika eneo la utafiti wa kina. "Pamoja na kuendelea kukua kwa kasi kwa sekta yetu ya madini, Nchi yetu imefanikiwa kufanya utafiti wa kina kwa asilimia 16 pekee. Hivyo, iwapo tutaongeza eneo kubwa litakalokuwa l...