Skip to main content

Posts

Showing posts from June 5, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MAVUNDE: USHIRIKIANO NA URUSI UTAONGEZA UTAFITI WA MADINI TANZANIA

  WAZIRI  wa Madini Nchini Tanzania Anthon Mavunde Leo June 5,2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Serikali ya Urusi kwenye sekta ya madini ukiongozwa na Naibu Waziri wa Maliasili(Madini) na Mazingira wa Shirikisho la Urusi, *Mh. Tetenkin Dmitry Dmitrievich*. “Pamoja na kuendelea kukua kwa kasi kwa sekta yetu ya madini, Nchi yetu imefanikiwa kufanya utafiti wa kina kwa asilimia 16 pekee. Hivyo, iwapo tutaongeza eneo kubwa litakalokuwa limefanyiwa utafiti, kutatanua wigo wa taarifa zaidi za mashapo ya madini na kuvutia zaidi wawekezaji, Eneo hili la utafiti tunaona ni fursa kubwa ya kuanza nayo katika kuimarisha mashirikiano yetu na Serikali ya Urusi kutokana na hatua kubwa mliyopiga hususan katika utafiti wa kijiolojia na teknolojia ya kisasa kupitia maabara zenye vifaa bora”  Tumezungumza juu uwepo wa Hati ya Makubaliano(MoU) baina ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) na Chuo Kikuu cha Urusi ambayo bado haijakamilika na kumwomba kuiwekea nguvu i...

DKT. MWIGULU NCHEMBA ATATUA MGOGORO WA ARDHI ULIDUMU MIAKA 41 NYOLOLO MUFINDI

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ametatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka 41 kati ya Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana  Mtume Nyololo wilayani Mufindi Mkoa wa Iringa na Familia ya   Yosefa Mgavilenzi ambaye ni msimamizi wa mirathi ya marehemu Michael Bakari Seveyage. Akihutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Igowole Mufindi Kusini, Waziri Mkuu alipokea malalamiko ya familia ya  Yosefa Mgavilenzi kuwa eneo lake lenye ukubwa wa ekari 107 limechukuliwa na Kanisa hilo bila fidia na aliomba Waziri Mkuu amsidie ili alipwe. Mapema wiki hii Waziri Mkuu alituma timu ya wataalamu kutoka ofisi yake ambao walikwenda katika kata ya Nyololo na kufanya vikao vya maridhiano na viongozi wa Kanisa Katoliki, familia ya Yosefa, Wazee, viongozi wa Kata ya Nyololo na  kijiji  cha Nyololo Shuleni walioko madarakani na wastaafu pamoja na wananchi.  Baada ya majadiliano yaliyochukuwa siku tatu pande mbili husika zilikubaliana kumaliza mgogoro kwa njia y...

MAKUSANYO MADINI YAVUKA LENGO, YAKUSANYA TRILIONI 1.27

✅️ *Sawa na Asilimia 105.8, Zikiwa Zimebaki siku 26 Kufunga Mwaka wa Fedha 2025/26* ✅️ *Watumishi Watakiwa Kuongeza Weledi Kufikia Sh Trilioni 1.4 Mwaka 2026/27* ✅️ *Watumishi  Watakiwa kuhudumia wananchi bila ubaguzi* *Na Mwandishi Wetu, Dodoma* WIZARA ya Madini imevuka lengo la ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 baada ya kukusanya Sh trilioni 1.27 hadi Juni 5, 2026, dhidi ya lengo la Sh trilioni 1.2, huku ikitarajia kufikia Sh trilioni 1.3 ifikapo  Juni 30, 2026. Kutokana na mafanikio hayo, watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake wametakiwa kuondokana na uzembe, kuongeza bidii na kufanya kazi kwa weledi ili kufikia lengo jipya la ukusanyaji wa Sh trilioni 1.4 lililowekwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Akizungumza katika kikao cha watumishi wote wa Wizara ya Madini na taasisi zake ambazo ni GST, TEITI, Tume ya Madini, STAMICO na TGC, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, amesema mafanikio yaliyopatikana yanapaswa kuwa chachu ya kuon...

WASIRA AWASILI KILIMANJARO, KWA ZIARA YAKE YA KIKAZI

Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Ndugu Stephen Wasira, amewasili leo mkoani Kilimanjaro kwa ziara rasmi ya kikazi ya siku 5 Mkoani humo. Ndg Wasira amepokelewa na viongozi mbalimbali wa chama wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Ndugu Patrick Boisafi, alipowasili Katika Ofisi za CCM Mkoani hapo  Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, Ndugu Wasira anatarajiwa kukutana na kuzungumza na viongozi na wanachama wa CCM ngazi zote ndani ya mkoa huo. Lengo ni kuimarisha mshikamano na kupata uelewa wa changamoto zinazowakabili. Kilele cha ziara hiyo kitakuwa tarehe 8 Juni, 2026 ambapo anatarajiwa kuongoza mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Same.

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NCHINI AKUTANA NA MAAFISA WA JESHI LA INDIA

 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa washiriki wa kozi kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa cha India walipotembelea Ofisi za iliyokuwa Makao Makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es Salaam leo tarehe 05 Juni 26. Akizungumza na washiriki wa kozi hiyo, Jenerali Mkunda amesisitiza kuendelea kwa ushirikiano wa kimafunzo kati ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na Jeshi la India ili kuwajengea uwezo kijeshi wanajeshi wa nchi mbili hizi. "Tunashuru kwa kuja kuitembelea Tanzania kwa ziara ya kimafunzo, hii inaonesha jinsi diplomasia ya kijeshi inavyochangia kuongeza weledi na ujuzi kijeshi. Naye, Mkuu wa msafara wa washiriki wa kozi hiyo Rear Admiral…amesema kuwa, kundi la washiriki wa kozi ya NDC India wamejionea jinsi JWTZ linavyoboresha mafunzo yake, na kupongeza maendeleo ya kimafunzo kwa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (Command and Staff Collage) kilichopo Duluti Jijini Arusha. Aidha, Rear Admiral…alipongeza juhudi za Serik...

WAZIRI MKUU ASISITIZA UTOAJI WA HAKI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa haki kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji kwa watumishi wa umma ili kuhakikisha huduma za Serikali zinatolewa kwa ufanisi, kwa wakati na kwa kuzingatia maslahi ya wananchi. Amesema hayo leo Ijumaa, Juni 5, 2026 alipokuwa akizungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa katika Jimbo la Isimani mkoani Iringa katika viwanja vya Isimani tarafani. Dkt. Mwigulu amesema haki za wananchi hazipaswi kucheleweshwa wala kunyimwa kwa sababu yoyote na kusisitiza kuwa kila anayestahili haki yake anapaswa kuipata kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa. “Haki si hisani. Tunataka anayestahili haki apewe haki yake. Serikali haitavumilia vitendo vya kupora au kuchelewesha haki za wananchi kwa sababu yoyote ile,” amesema. Aidha, Waziri Mkuu amesema watumishi wa umma wanapaswa kutambua kuwa nafasi walizonazo ni dhamana ya kuwatumikia wananchi na kwamba huduma zinazoweza kutolewa kwa siku hiy...

TTB YALENGA KUVUTIA WATALII 134,000 KUTOKA URUSI KILA MWAKA

  Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg, Urusi  BODI ya Utalii Tanzania (TTB) inajipanga kumega keki ya utalii inayotengenezwa na Urusi kwa lengo la kulipatia taifa zaidi ya dola za Marekani 500 kwa mwaka. Zaidi ya wananchi milioni 13.4 wa Urusi hutalii sehemu mbalimbali duniani na kutokana na kuwa watumiaji wazuri wa vipato vyao, Tanzania ikipata angalau asilimia 1 ya watu hao ambacho ni sawa na watu 134,000 ambao wataingiza dola milioni 500. Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la Petersburg (SPIEF’26) linaloendelea mjini hapa. Mafuru alisema katika mikakati hiyo wanataka katika miaka 10 ijayo kufikisha watalii mara mbili ya hao na hivyo kuliingizia pato taifa la dola za Marekani bilioni moja. Akiwa katika banda la Tanzania katika jukwaa hilo alisema anafurahi kwa Rais Samia kuendelea kuelekeza maono kwa vitendo katika kusaka wawekezaji. Pia kufungua fursa za Watanzania kwa ziara zinazojumuisha watendaji wakuu wa maen...

RAIS SAMIA AINADI TANZANIA KATIKA KONGAMANO KUBWA LA LA KIMATAIFA NCHINI URUSI

 Na Beda Msimbe, TBN, St Petersburg       Rais Samia Suluhu Hassan leo anahitimisha ziara yake nchini Urusi kwa kushiriki katika kongamano la kibiashara kati ya Tanzania na Urusi sanjari na Jukwaa la Kimataifa la Biashara la St Petersburg.         Katika jukwaa hilo Rais Samia anatarajiwa kuinadi Tanzania katika sekta za uwekezaji na biashara.              Ziara ya Rais Samia imekuwa na mafanikio makubwa hasa hakikisho la ushiriano wa karibu na Urusi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ya uendelezaji wa rasilimaliwatu na ukuzaji wa teknolojia.   Ziara hiyo katika taifa lenye nguvu kubwa kiteknolojia, uchakataji na uzalishaji kwenye kilimo au viwandani imekuja wakati Tanzania inajiandaa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kulifanya taifa kuwa na pato la dola trilioni moja kwa mwaka.                   Kwa sasa serikali ime...

SERIKALI YAZINDUA KITUO CHA OPERESHENI NA MAWASILIANO YA DHARURA MWANZA

 Na, mwandishi wetu – Mwanza SERIKALI imezindua rasmi Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa wa Mwanza, hatua inayolenga kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa na majanga katika mkoa huo. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo leo tarehe 05 Juni, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, amesema kituo hicho ni nyenzo muhimu katika kufuatilia na kudhibiti matukio ya dharura kwa ufanisi zaidi.  Amesema kupitia kituo hicho, mkoa unaweza kufuatilia matukio ya dharura kwa karibu, kukusanya na kuchambua taarifa kwa wakati pamoja na kuimarisha mawasiliano kati ya wadau mbalimbali wa usimamizi wa maafa. “Kupitia kituo hiki, taarifa muhimu zinafika kwa mamlaka husika kwa haraka ili kuwezesha maamuzi stahiki kufanyika kwa wakati,” anasema Mhe.Mtanda. Ameongeza kuwa kituo hicho kinaunganishwa moja kwa moja na Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, hatua inayorahisisha mtiririko wa taarifa na kuimarisha uratibu wa shughuli za kukab...