Skip to main content

Posts

Showing posts from August 18, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Watumishi ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Wakumbushwa kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amewakumbusha  watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kufanya kazi na kutekeleza majukumu yao  kwa ufanisi  na ushirikiano ili kuleta matokeo chanya zaidi. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametoa rai hiyo wakati akizungumza katika kikao na Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali kilichofanyika Jijini Dodoma tarehe 18 Agosti, 2025. *“Niwakumbushe watumishi kuendelea kutekeleza majukumu  kwa ufanisi na ushirikiano, tuendelee kuzingatia Weledi na Ubora.”* Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametumia kikao hicho kuwafahamisha rasmi Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa iliyokuwa Divisheni ya Uandishi wa  Sheria imekuwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na imeanza kutekeleza majukumu yake kuanzia tarehe 1 Julai, 2025, ambapo ameeleza kuwa lengo la maboresho hayo ni kuongeza tija katika utoaji wa huduma za Uandishi wa Sheria. *“Msije mkafik...

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Kuboresha Sheria Kuelekea Utekelezaji wa Dira 2050

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeanza kufanya maboresho ya Sheria mbalimbali  ili kurahisisha utekelezaji wa Dira 2050, Hayo yamesemwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lkilchofanyika tarehe 18 Agosti, 2025 Jijini Dodoma. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi Mwanasheria Mkuu wa Serikali na  Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa Serikali imeanza mkakati wa kufanya maboresho katika sheria ili kuhakikisha kuwa, sheria, sera, mipango, malengo na mikakati mbalimbali pamoja na vigezo na viashiria vilivyowekwa vya upimaji wa matokeo ya kiutendaji wa Watumishi wa umma, vinafungamanishwa na malengo na shabaha ya Dira ya 2050.  *"Ofisi yetu, inao wajibu wa kupanga, kuratibu, kutekeleza michakato ya tathmini na mapitio ya sheria za Bunge na sheria ndogo za Mamlaka za Ser...

Tanesco Mara Yahamasisha Nishati Safi ya Kupikia

 Na Ada Ouko, GMTV Musoma. WAKAZI wa Manispaa ya Musoma wameaswa kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuachana na matumizi ya nishati isiyo safi kutokana na athari zake kwa binadamu na mazingira. Wito huo umetolewa Agosti 17,2025 na Afisa Uhusiano na huduma(TANESCO ) mkoa wa Mara Joyce Makori wakati akitoa elimu juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwenye uwanja wa Mara sekondari kwenye mkesha wa mbio za Mwenge wa uhuru. " Tumekuja hapa na majiko ya umeme na kufanya mapishi mubashara kwa wananchi kwa kuonyesha kwa mfano ni jinsi gani ukitumia majiko ya umeme unaweza ukatumia umeme kidogo na ukapika chakula vizuri kwa gharama nafu pia kukaokoa muda" Amesema TANESCO mkoa wa Mara ina muunga mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Hassan na kwamba majiko ya umeme yamefanyiwa utafiti na wataalam wa Tanesco. "Watafiti wetu wa Tanesco wamegundua kuwa unapopika nyama au maharage kilo moja kwa kutumia nishati ya umeme kwa majiko haya unaset...

Gachagua ataka Trump amlete balozi ‘asiyebembelezana’ na Ruto

 ALIYEKUWA Naibu Rais Rigathi Gachagua sasa anamtaka Rais wa Marekani Donald Trump amteue balozi ambaye hapendelei utawala wa Rais William Ruto. Akiongea wakati wa mahojiano Jiji la Kansas, Marekani, Bw Gachagua alisema Rais Trump atasaidia kusafisha Kenya iwapo tu atamteua balozi ambaye anapigania utekelezaji wa sheria na kuheshimiwa kwa haki nchi inapoelekea uchaguzi mkuu wa 2027. Kwa mujibu wa Bw Gachagua, Marekani inastahili kutuma balozi mwenye sifa kama Smith Hempstone ambaye alihudumu nchini kati ya 1989-1993. “Tunamwomba Rais Trump kuwa anapomteua balozi mpya Kenya, amteue yule mwenye sifa kama za Hempstone ambaye alisaidia Kenya wakati utawala wa enzi hizo ulikuwa ukishiriki ukiukaji wa haki za kibinadamu na kulemaza demokrasia. Tutafurahi sana tukimpata balozi kama Hempstone,” akasema Bw Gachagua. Marehemu Balozi Hempstone alikuwa mwiba wakati wa utawala wa Kanu na ni kati ya walioshinikiza kukumbatiwa kwa mfumo wa vyama vingi katika uchaguzi mkuu wa 1992. Kauli ya Bw Gac...