Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amewakumbusha watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kufanya kazi na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na ushirikiano ili kuleta matokeo chanya zaidi. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametoa rai hiyo wakati akizungumza katika kikao na Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali kilichofanyika Jijini Dodoma tarehe 18 Agosti, 2025. *“Niwakumbushe watumishi kuendelea kutekeleza majukumu kwa ufanisi na ushirikiano, tuendelee kuzingatia Weledi na Ubora.”* Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametumia kikao hicho kuwafahamisha rasmi Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa iliyokuwa Divisheni ya Uandishi wa Sheria imekuwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na imeanza kutekeleza majukumu yake kuanzia tarehe 1 Julai, 2025, ambapo ameeleza kuwa lengo la maboresho hayo ni kuongeza tija katika utoaji wa huduma za Uandishi wa Sheria. *“Msije mkafik...
Marato tv - Sauti ya Jamii