Skip to main content

Posts

Showing posts from August 3, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wizara ya Kilimo Iziweshe Taasisi Kupata Zana za Kisasa - Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo iweke utaratibu wa kuziwezesha taasisi zinazojihusisha na kilimo kwa kuzipatia zana za kisasa za kilimo ili kukuza sekta hiyo. Amesema kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza tija katika shughuli za kilimo zinazofanywa na taaaisi hizo. “Mitambo hii ya kupandia, kuvunia pamoja na umwagiliaji ina gharama kubwa sana, lakini Wizara yetu ya Kilimo ikiweka utaratibu mzuri wa kuziwezesha hata kwa mkopo itazisaidia kuzalisha kwa tija.” Ametoa agizo leo (Jumapili, Agosti 03, 2025) wakati akizungumza na wadau wa ushirika na wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Ushirika, kwenye viwanja vya maonesho ya NaneNane, Nzughuni, jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wakulima kwa mwaka 2025. Amesema taasisi kama Magereza, JKT ambazo zinafanya shughuli za kilimo zikipatiwa zana hizo kwa mikopo, zitawawezeshwa kuwa na teknolojia za kisasa jambo ambalo wasingeweza kul...

Majaliwa awapongeza vijana wanaofuga samaki kwa vizimba kwa mkopo wa TADB

Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAZIRI  Mkuu Kasim Majaliwa, amewapongeza  vijana wanaojiajiri kwa kufuga samaki kwa kutumia vizimba na kutaka wengine waige mfano huo. Alitoa pongezi kwa vijana hao leo alipotembelea banda la Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB na kukuta simumizi za vijana hao ambao wameweza kufuga samaki na kuingiza faida ya mamilioni. Majaliwa alisema vijana hao wanatakiwa kushikwa mkono ili waweze kusonga mbele kwa kuwa na mtaji mkubwa utakaowawezesha kuuza samaki kwenye soko la kimataifa. Alisema vijana hao watumike kama mfano kwa vijana wengine kuingia kwenye ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ili waondokane na umaskini kwa kujiajiri wenyewe kama vijana hao  wa VIJANA NGUVU KAZI MWANZA. Naye Mkurugenzi wa Mipango, Ushauri na Uhusiano wa Taasisi Mkani Waziri, alimweleza Waziri Mkuu kuwa mradi huo ulizinduliwa mwaka jana na Rais Samia Suluhu Hassan. Alimweleza kuwa kupitia mradi huo, vijana wamekopeshwa shilingi milioni 137  ukiwa ni mkopo usio na riba ...

Majaliwa Aiagiza Wizara ya Kilimo Kukuza Teknolojia za Umwagiliaji Nchini

  📍NIRC:Dodoma  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kasim Majaliwa, amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Dkt.Gerald Mweli kuhakikisha kuwa Wizara hiyo, kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, inashirikiana na sekta nyingine za umma ili kuhimiza matumizi ya teknojia za kisasa za Umwagiliaji, ikiwa ni pamoja kuhamasisha uwekezaji kutoka kwa wadau wa sekta binafsi wenye uwezo wa kuleta teknojia hizo nchini. Pia Majaliwa amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa kwa kuhakikisha kunakuwapo mitambo na  teknolojia za kisasa za Umwagiliaji katika maonesho hayo, ambazo zitatumika katika kaboresha sekta ya kilimo nchini na matumizi mengine ikiwemo viwanja vya michezo. Waziri Mkuu Majaliwa amesema hayo katika maonesho ya nanenane 2025, alipotembelea eneo la Umwagiliaji ikiwemo kijiji cha mitambo ya Umwagiliaji, lengo likiwa ni kukagua mitambo mbalimbali na uwekezaji wa serikali uliofanywa katika sekta hiyo. Majaliwa amesema, kazi kub...

NEMC yataka uvuvi unaozingatia usimamizi na uhifadhi wa mazingira

Na Mwandishi Wetu, Dodoma BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limewakumbusha wawekezaji kuhakikisha wanakuwa na cheti cha tathmini ya mazingira (EIA) kabla ya kufanya uwekezaji wowote. Wito huo umetolewa leo jijini Dodoma na Kaimu Meneja wa NEMC Kanda ya Kati-Dodoma, Novatus Mushi, wakati akitoa elimu kwa umma kwenye maonyesho ya wakulima yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni Dodoma. Alisema sheria inawataka wawekezaji wote kuhakikisha wanakuwa na EIA na wale ambao wamekuwa wakikaidi wamekuwa wakitozwa faini kwa ukiukwaji huo wa sheria ya mazingira. Alisema NEMC inatoa kipaumbele kutoa elimu kwa umma kabla ya kufanya ukaguzi wa kuwabaini watu wanaokiuka sheria ya mazingira kwenye maeneo mbalimbali nchini. “Hapa kwenye banda letu tunatoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria ya mazingira na tumekuwa tukifanya ukaguzi wa mara kwa mara kuhakikisha kina uwekezaji unaofanywa unazingatia sheria na wale wanaokutwa wamekiuka sheria taratibu za sheria zi...