Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI OMAR ASHUKURU IMF KWA USHIRIKIANO WA MUDA MREFU NA TANZANIA


 Na. Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amelishukuru Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa mchango wake kwa Tanzania tangu kuanza kwa ushirikiano kati yake na Shirika hilo, akieleza kuwa ushirikiano huo umeendelea kuwa muhimu katika kuimarisha uchumi na utekelezaji wa ajenda za maendeleo nchini.

Ametoa Shukran hizo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi mpya wa IMF nchini Tanzania, Bi. Jana Bricco, ambaye ameanza rasmi majukumu yake nchini, ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano kati ya Tanzania na IMF, ambao umedumu kwa zaidi ya miongo sita tangu uanzishwe miaka ya 1960.


Mhe. Balozi Omar amesema Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano na IMF katika kufanikisha ajenda ya maendeleo ya Tanzania, ikiwemo utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na mwelekeo wa kimkakati wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano unaofuata ambayo ni maeneo yenye manufaa kwa pande zote na yanayochangia utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya Tanzania.

“Tumekuwa na ushirikiano na IMF kwa muda mrefu, tangu miaka ya 1960 hadi leo, na tumeendelea kushirikiana katika maeneo mbalimbali yanayolenga kuimarisha uchumi wa nchi na kufanikisha ajenda yetu ya maendeleo,” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa Tanzania inathamini ushirikiano huo, hususan katika kufuatilia mwenendo wa ukuaji wa uchumi, sera za fedha na sera za kiuchumi (monetary policy na fiscal policy), pamoja na matokeo ya utekelezaji wa sera hizo.

Mhe. Balozi Omar alisema wataendelea kutazamia kwa pamoja maendeleo ya sekta binafsi na mwenendo wa bei za bidhaa na huduma, ikiwemo mfumuko wa bei (inflation), maeneo ambayo yameendelea kuwa sehemu muhimu ya majadiliano kati ya Tanzania na IMF.

Aidha, Mhe. Balozi Omar ametoa wito kwa Mwakilishi huyo mpya wa IMF kutembelea maeneo mbalimbali nchini ili kupata fursa ya kujionea kwa vitendo maendeleo yanayotekelezwa na Serikali, hususan miradi mikubwa ya kimkakati, kama vile Bwawa la kuzalisha Umeme la Mwalimu Julius Nyerere.

“Mbali na miradi ya kimkakati, nakukaribisha kutembelea maeneo ya utalii na uzalishaji, hususan katika sekta ya kilimo na maeneo mengine yenye mchango mkubwa katika shughuli za kiuchumi nchini, na zitakusaidia kupata uelewa mpana zaidi kuhusu fursa, maendeleo na changamoto zilizopo nchini, hivyo kuwezesha majadiliano na ushirikiano wenye tija zaidi kati ya Tanzania na IMF.” alisema Mhe. Balozi Omar

Kwa Upande wake Mwakilishi mpya wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) nchini Tanzania, Bi. Jana Bricco, ameipongeza Tanzania kwa kukamilisha kwa mafanikio Mpango wa Extended Credit Facility (ECF) inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii na Resilience and Sustainability Facility (RSF) ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, mafanikio ambayo yamechangiwa na kuimarika kwa utulivu wa uchumi jumla, uendelevu wa bajeti na kupungua kwa kiwango cha deni la Taifa. 

Bi. Bricco amesema mafanikio hayo yalibainishwa na kuthaminiwa katika kikao cha Bodi ya IMF, na kukamilika kwa programu hiyo kunatoa fursa ya kuanza ukurasa mpya katika uhusiano kati ya Tanzania na IMF, utakaojikita zaidi katika mashauriano ya sera, ufuatiliaji wa uchumi na kujenga uwezo wa kitaalamu,


“Kukamilika kwa ECF-RSF hakumaanishi mwisho wa ushirikiano kati ya Tanzania na IMF, bali ni fursa ya kuubadilisha na kuuimarisha uhusiano huo kulingana na hatua mpya ya maendeleo ya Tanzania, huku IMF ikiendelea kuwa mshirika katika juhudi za kuimarisha ustawi wa uchumi, uendelevu wa sera na kufanikisha matarajio ya maendeleo ya Taifa kwa mwaka 2050” alisema Bi. Bricco.


Aliongeza kuwa IMF iko tayari kuendelea kushirikiana na Serikali katika kipindi kijacho kwa kutoa ushauri wa sera unaoendana na mahitaji ya nchi pamoja na msaada wa kujenga uwezo katika maeneo yatakayopewa kipaumbele katika utekelezajinwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


“IMF inaona nafasi kubwa ya kuendelea kuunga mkono utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, malengo na maeneo yaliyolengwa katika programu zilizokamilika yana mwingiliano mkubwa na matarajio ya Tanzania ya kujenga uchumi imara, shindani na wenye uwezo wa kutoa fursa zaidi kwa wananchi” alisema Bi. Bricco 


Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Kaimu Katibu Mkuu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, Kamishna Msaidizi wa Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Robert Mtengule, Kamishna Msaidizi Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. Juma Mkabakuli na maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha na IMF.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...