Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

ZIARA YA MAGANYA ILIVYOTUMIKA KUMPIGISHA "SHOTI" MBUNGE WAITARA TARIME


 MBUNGE wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara, amemtupia lawama Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tarime, akidai kuwa uongozi huo uliwatelekeza wajumbe wa chama waliokuja kutoka kata mbalimbali za wilaya hiyo kwa kushindwa kuwaandalia mahitaji muhimu, ikiwemo nauli, chakula na vinywaji.

Waitara ametoa kauli hiyo mara baada ya kushiriki kongamano la Bima ya Afya pamoja na changizo la ujenzi wa bweni lililoandaliwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Gati Chomete, akisema alilazimika kusafiri usiku kutoka Dodoma ili kushiriki shughuli hiyo kama sehemu ya kuonesha mshikamano na umoja miongoni mwa wananchi wa Mkoa wa Mara.

Amesema alifika katika shughuli hiyo kwa sababu agenda ya ujenzi wa bweni ni muhimu kwa watoto, kwani itawapa mazingira bora ya kujifunza na kujisomea, huku akisisitiza kuwa viongozi wa Mara wanapaswa kushirikiana katika shughuli zenye manufaa kwa wananchi.

“Mimi nimetoka Dodoma, nimesafiri usiku usiku kuja hapa kwenye changizo hili kwa sababu kuna agenda muhimu ya kujenga bweni kwa ajili ya watoto. Nimekuja kuonesha mshikamano na umoja wa watu wa Mara,” amesema Waitara.

Hata hivyo, Waitara ametumia nafasi hiyo kueleza kutoridhishwa kwake na namna kikao cha CCM Wilaya ya Tarime kilivyoendeshwa, akidai kuwa wajumbe kutoka kata mbalimbali waliitwa mjini Tarime kupitia utaratibu wa chama, lakini walipofika hawakupewa msaada wa mahitaji muhimu.

Amesema kikao hicho kilihusisha wajumbe zaidi ya 400 pamoja na wazee wa chama kutoka maeneo mbalimbali, ambao walifika katika ukumbi wa CMG Hotel tangu asubuhi.

Kadhalika, amesema  kutokana na wajumbe hao kuitwa rasmi na chama kupitia Katibu wa Wilaya, alitarajia uongozi wa chama ungetoa ushirikiano kwa kuwaandalia chakula, vinywaji na hata nauli, badala ya kuwaelekeza kwenda kwa ofisi ya mbunge.

Waitara amedai kuwa licha ya yeye kuwa nje ya Tarime kwa majukumu ya kikazi Dodoma, taarifa ilitolewa kwamba angehusika kuwasaidia wajumbe kutoka Tarime Vijijini, jambo ambalo alisema lilimweka katika hali ngumu kutokana na idadi kubwa ya wajumbe.

“Wajumbe walialikwa na chama. Tungetegemea chama kiwape support, maana wamekuja hapa kwa mwaliko wa chama. Lakini wanaambiwa wajitegemee. Mimi nilikuwa Dodoma na nilishasema sitaweza kuwepo, lakini nilisema nitachangia kwa uwezo wangu,” amesema.

Mbunge huyo pia ameeleza kushangazwa na uamuzi wa kuwaelekeza wajumbe kutoka Tarime Vijijini kwenda kwa Katibu wa Mbunge ili kupata msaada, akidai kuwa hatua hiyo inaweza kujenga taswira kwamba yeye kama mbunge ameshindwa kuwahudumia wananchi wake.


Amesema wajumbe hao walitoka maeneo mbalimbali ya Jimbo la Tarime Vijijini, hivyo kuwahudumia wote kwa muda mfupi kunahitaji maandalizi makubwa na rasilimali za kutosha.

Waitara aliongeza kuwa anachopinga si wajumbe kupewa msaada, bali utaratibu uliotumika ambapo watu waliitwa na chama kisha jukumu la kuwahudumia likaelekezwa kwa mbunge.


“Maana yake ni nini? Anataka wale wajumbe wamtukie mbunge kwamba mbunge anaonekana kama ameshindwa kuwahudumia watu wake. Lakini yeye na wenzake wanapata nafasi ya kujisafisha. Hiki ni kitendo cha kuchonganisha watu na kuvunja mshikamano,” amesema.


Aidha, Waitara amedai kuwa changamoto hiyo imekuwepo kwa muda mrefu katika uhusiano wake na Katibu huyo wa Wilaya, akisema amekuwa akivumilia matendo anayodai yamekuwa yakilenga kumdhoofisha kisiasa.


Amedai kuwa Katibu huyo aliwahi kumtangaza kuwa hatakuwa mbunge wa Tarime Vijijini na hata kusema hamtambui, lakini licha ya tofauti hizo, yeye ameendelea kufanya kazi na wananchi pamoja na viongozi wengine.


“Amekuwa akinishughulikia sana, lakini nimevumilia. Sasa mwaka huu kuna uchaguzi, anaanza mambo haya kwa sababu anataka watu wangu waanze kuteseka ili lawama zimwangukie mbunge,” amesema.

Waitara pia amekosoa hali ya baadhi ya miundombinu ya chama wilayani Tarime, akidai kuwa baadhi ya ofisi na vibanda vya chama havijaoneshwa wazi matumizi ya mapato yake, huku akitaka kuwepo kwa uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji wa chama.

Akizungumzia hatua za kuchukua, Waitara amesema ataandika malalamiko rasmi ndani ya chama na kutaka suala hilo lifanyiwe kazi, akisisitiza kuwa hataki tena fedha zake zitumike katika mazingira ambayo anaona hayana ushirikiano na uongozi wa chama wa wilaya.

“Nimeishatangaza. Wajumbe kutoka Tarime Vijijini wakiitwa kwenye vikao kuja Tarime mjini, kama mimi sijaalikwa au kupewa taarifa kupitia Katibu wa Mbunge, mtu yeyote asinisumbue. Kama nitakuwa na uwezo wangu, nitafanya kazi yangu moja kwa moja na wananchi na viongozi wanaoniheshimu na kutambua nafasi yangu,” amesema.

Waitara amesema licha ya tofauti hizo, ataendelea kufanya kazi na wananchi wa Tarime Vijijini, akisisitiza kuwa lengo lake ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma na maendeleo bila kuathiriwa na tofauti za kisiasa ndani ya chama.

Juhudi za kumpata katibu wa CCM wilaya ili aweze athibitishe madai haya hazikuzaa matunda baada ya simu yake ya mkononi kutopatikana na kwamba juhudi zaidi za kumtafuta zinaendelea ili aweze kuelezea madai haya.






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...