Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WALALAZE: MIAKA 30 YA TRA, TUNAJIVUNIA MAENDELEO, UWAZI, UHUSIANO MZURI, NA MAGEUZI YA KIMIFUMO


 NA: MWANDISHI WETU, DODOMA

Ikiwa ni takribani miaka 30 imepita tangu ianzishwe Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Julai 1, 1996, Mamlaka hiyo inajivunia maendeleo, uwazi, mageuzi na mabadiliko chanya ya kimifumo yaliyofanyika ambayo yamekuwa chachu ya kufikia malengo ya Mamlaka hiyo na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Akizungumza kuhusiana na mafanikio hayo, Juni 28, 2026, Jijini Dodoma, Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA,  Paul Walalaze, anasema imekuwa ni miaka 30 ya mafanikio mengi na Mamlaka inajivunia utendajikazi na ushirikiano mkubwa wanaoupata kutoka kwa walipakodi na wananchi katika ujenzi wa taifa.

"Kama ambavyo TRA inawajibika kukusanya kodi, katika miaka hii 30, tumeweza kuongeza makusanyo kutoka shilingi bilioni 531 kwa mwaka wa fedha 1996/1997 hadi trilioni 32 mwaka 2025/2026, ongezeko hili ni kubwa na ndiyo maana serikali inafanya mambo makubwa ya kimaendeleo kwa wananchi wake, kwani fedha za kufanya hayo zipo," amesema Walalaze.

Aidha, Walalaze anasema, TRA imefanikiwa kuwafikia wanafunzi, walipakodi na wananchi wengi kuwapa elimu ya kodi. 

"TRA tunakwenda walipo wadau wetu, yaani shuleni, vyuoni, sehemu za kazi, viwandani na kwenye biashara ili kuwapa elimu. Pia tunashirikiana na taasisi za elimu kufundisha masuala ya kodi, kutumia vipeperushi, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, hii yote ni kuhakikisha kila raia anakuwa na uelewa wa masuala ya kodi na ashiriki katika kulipa kodi," amesema.

Sambamba na hilo, Meneja huyo wa Elimu ya Mlipakodi, anasisitiza kuwa, Mamlaka ya Mapato imeimarisha matumizi ya teknolojia katika utendaji na usimamizi wa kodi ili kufikia malengo yaliyowekwa.

"Kwa kiwango kikubwa sana, Mamlaka imehama kutoka kwenye matumizi ya karatasi na sasa tupo kidijitali zaidi. Mathalani, usajili wa walipakodi, malipo ya kodi, utoaji wa risiti, masuala ya forodha na mengine mengi yanafanyika kwa njia ya mtandao."

"Tulipoanza kutumia teknolojia, baadhi walikuwa na hofu, lakini leo, walipakodi wenyewe wanafurahia kwani hawana ulazima wa kufikia katika ofisi za TRA kuhudumiwa, wanafanya shughuli zao kule kule walipo, na Mamlaka inapata taarifa zao," amesema.

Katika hatua nyingine, Walalaze anasema, katika miaka 30, Mamlaka inajivunia kuongezeka uwazi na uwajibikaji ambao umekuwa nyenzo muhimu ya kufikia malengo na maendeleo.

"Sasa hivi hakuna janjajanja, utendajikazi na shughuli za kikodi zinafanyika kwa uwazi, na uwazi huu umeongeza uwajibikaji na uadilifu kwa watendaji wa Mamlaka na walipakodi pia," amesisitiza.

Vilevile, Mamlaka imefanikiwa kujenga uhusiano mzuri kati yake na walipakodi. Anasisitiza kuwa, kumekuwa na mafanikio ya kujenga uhusiano mzuri ambao umekuwa chachu ya ongezeko la makusanyo ya kodi, kwani meza ya mazungumzo ipo na inatumika vyema kufikia muafaka wa ulipaji kodi.

"Eneo la uhusiano mzuri limefanikiwa sana hasa kufuatia maelekezo ya Mheshimiwa Rais wetu, Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye anasisitiza majadiliano yachukue nafasi na kuachana na matumizi ya mabavu katika ukusanyaji wa kodi, na hapa niseme tumefanikiwa sana, na tija yake imeakisi katika ongezeko la mapato," amesema Walalaze.

Mafanikio mengine, ni kuimarika kwa mazingira ya biashara na uwekezaji. Walalaze anasisitiza kuwa wafanyabiashara na wawekezaji ni mashahidi wa namna Mamlaka ilivyoweka mazingira mazuri ya ufanyikaji wa shughuli za biashara na uwekezaji, na hili limesaidia kuongezeka kwa idadi ya wafanyabiashara ambao ni chachu ya kukuza uchumi na maendeleo nchini.

Kwa mwaka wa fedha 2026/2027, TRA inapaswa kukusanya shilingi trilioni 36.99 ili kufanikisha bajeti nzima ya serikali ya shilingi trilioni 62.33, hivyo TRA inahimiza walipakodi na wananchi kwa ujumla kutimiza wajibu wa kulipa kodi kwa hiari ili kufikia malengo ya serikali ya kukuza uchumi na kuboresha ustawi wa wananchi.

Ikumbukwe kuwa, Julai 1, 2026, Rais Dk. Samia atatoa tuzo kwa walipakodi mahiri kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa walipakodi katika ujenzi wa taifa na kujenga motisha kwa walipakodi kuendelea kulipa kodi.

Sambamba na hilo, Walalaze ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi, Julai 2, katika uwanja wa KMC Complex, ambapo kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya timu ya TRA United na URA FC kutoka Uganda, ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya miaka 30 ya mafanikio kwa kuzingatia TRA inashirikiana na mamlaka nyingine za ukusanyaji kodi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Katika mechi hiyo, hakuna kiingilio, yaani ni bure.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...