Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CHALAMILA ATUMIA SHERIA HIZI KUWAPELEKA WENYE MABASI STENDI YA MAGUFULI


 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka wamiliki na waendeshaji wa mabasi ya mikoani yanayofanya shughuli za usafirishaji katika maeneo ya katikati ya jiji kurejesha huduma zao katika Stendi Kuu ya Mabasi ya Magufuli, Ubungo, akiwapa hadi Jumatatu, Agosti 17, 2026, kutekeleza agizo hilo.

Chalamila amesema hatua hiyo inalenga kupunguza msongamano wa magari katikati ya jiji, kurejesha utaratibu wa matumizi ya vituo rasmi vya mabasi na kuhakikisha fursa za kiuchumi zinawafikia pia watoa huduma wengine wa usafiri, wakiwemo waendesha daladala, mabasi ya mwendokasi, bajaji na bodaboda.

Amesema Dar es Salaam ina Stendi ya Magufuli iliyojengwa kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 80 na yenye uwezo wa kuhudumia mabasi mengi kwa wakati mmoja, hivyo hakuna sababu kwa mabasi makubwa ya mikoani kuendelea kuzagaa katika maeneo ya katikati ya jiji, ikiwemo Shekilango na maeneo yanayounganisha barabara kuelekea Magomeni.

“Stendi yetu ile imejengwa kwa zaidi ya bilioni 80. Ni stendi ambayo ni bora na pengine kuliko stendi yoyote Tanzania. Inaweza kuchukua magari mengi kwa pamoja. Lakini kwa bahati mbaya sana, mabasi mengi hayako pale,” amesema Chalamila.


Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, kuna kampuni sita zilizopewa vibali maalum vya kuendesha huduma za mabasi katika maeneo mengine ya jiji, ikiwemo kuwa na vituo vidogo katika maeneo yaliyokubaliwa, lakini kampuni ambazo hazina vibali hivyo hazipaswi kuendelea kutumia vituo vilivyo nje ya Stendi ya Magufuli.

“Wito wangu, kuanzia leo, Agosti 12, 2026, mpaka kufikia tarehe 17, wale wote ambao hawana vibali vya ku-operate stendi zao katikati ya mji, warudishe mabasi yao Ubungo, Stendi ya Magufuli,” amesema.

Agizo hilo linaendana na masharti yaliyowekwa katika Sheria Ndogo za Vituo vya Mabasi na Maegesho ya Vyombo vya Moto za Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo za mwaka 2022, ambazo zinaweka utaratibu wa matumizi ya vituo vya mabasi katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 5(1) cha Sheria Ndogo hizo, Halmashauri ina wajibu wa kuanzisha vituo vya mabasi yanayofanya shughuli zake ndani ya eneo la Manispaa ya Ubungo, yakiwemo mabasi yanayotoka nje ya Halmashauri na yanayoingia ndani yake kwa ajili ya kupakia na kushusha abiria na mizigo.

Aidha, Kifungu cha 6(1) kinaweka wajibu kwa kila mmiliki au msimamizi wa mabasi yanayotoka au kwenda mikoani na nchi jirani kuingia katika eneo lililotengwa na Halmashauri kwa ajili ya kupakia na kushusha abiria na mizigo.

Sheria hiyo pia inaweka zuio kwa vituo visivyo rasmi, ambapo Kifungu cha 6(2) kinakataza mtu, mmiliki wa chombo cha usafiri au taasisi kuanzisha kituo cha mabasi, kupakia au kushusha abiria na mizigo katika eneo ambalo halijatengwa au kutambuliwa na Halmashauri kwa ajili ya shughuli hizo.

Hata hivyo, sheria inatambua uwepo wa vibali maalum, ambapo Kifungu cha 6(3) kinaeleza kuwa, isipokuwa kwa kibali maalum kutoka Halmashauri, mabasi yote yanatakiwa kuanza safari zake katika stendi iliyotengwa. Kifungu hicho ndicho kinachoeleza msingi wa tofauti kati ya kampuni zilizopewa ruhusa maalum na zile ambazo hazina kibali hicho.

Chalamila amesema mfumo unaokusudiwa ni mabasi makubwa ya mikoani kuishia Stendi ya Magufuli, kisha abiria wanaohitaji kwenda maeneo ya katikati ya jiji watumie huduma nyingine za usafiri zinazowaunganisha na maeneo wanayokwenda.

Amesema serikali tayari imeunganisha huduma ya Mwendokasi na Stendi ya Magufuli, hivyo abiria wanaweza kuendelea na safari zao kupitia usafiri wa mijini badala ya mabasi makubwa kuingia katikati ya jiji.

Amefananishia mfumo huo na usafiri wa anga, akisema abiria anayesafiri kwa ndege kwenda Kilimanjaro na kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro anaweza kutumia shuttle au usafiri mwingine kwenda Arusha au Moshi, badala ya ndege kuingia moja kwa moja katikati ya miji hiyo.

Kwa mantiki hiyo, Chalamila amesema mabasi makubwa yanapaswa kuwasafirisha abiria hadi Stendi ya Magufuli, ambako wanaweza kuunganisha safari zao kwa kutumia Mwendokasi, daladala, bajaji, bodaboda na huduma nyingine za usafiri.

Amesema kuendelea kwa mabasi makubwa kuingia katikati ya jiji kunaongeza foleni na wakati huohuo kuwaondolea fursa watoa huduma wengine wa usafiri ambao wanategemea abiria wanaoshuka katika vituo vikuu.

“Kitendo cha kuingiza mabasi katikati ya mji maana yake moja ni kusababisha foleni. Jambo la pili ni kunyang’anya fursa za bodaboda, bajaji, daladala, mwendokasi na kadhalika,” amesema.

Msimamo huo pia unaendana na Kifungu cha 6(7) cha Sheria Ndogo hizo, kinachokataza kufungua ofisi, kituo au kufanya biashara inayofanana na shughuli zinazofanywa katika kituo cha mabasi katika eneo lote la Halmashauri.

Sheria hizo pia zinaweka utaratibu wa maegesho ya vyombo vya usafiri. Kifungu cha 13(1) kinakataza kuegesha gari au chombo chochote cha usafiri katika maeneo ambayo hayajatengwa kwa ajili ya maegesho au kuegesha kwa namna isiyoruhusiwa.

Kwa mujibu wa masharti hayo, Halmashauri inaweza kukokota au kufunga chombo cha usafiri kilichoegeshwa isivyostahili na kumtaka mmiliki kulipa faini pamoja na gharama zinazohusiana na uvutaji na utunzaji wa chombo hicho.

Akizungumzia mabasi yanayohitaji kufanyiwa matengenezo, Chalamila amesema hakuna tatizo kwa mabasi kwenda gereji, lakini amesisitiza kuwa magari hayo hayapaswi kupaki au kufanyia matengenezo katika uso wa barabara kuu na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara.

Sheria Ndogo hizo pia zinaweka adhabu kwa wanaokiuka masharti yake. Kwa mujibu wa Kifungu cha 18, makosa yanayoweza kuchukuliwa hatua ni pamoja na kuegesha chombo cha usafiri katika eneo lisiloruhusiwa, kuingia katika kituo cha mabasi bila kulipa ushuru, kufanya shughuli zisizoruhusiwa na kuzuia maafisa au mawakala wa Halmashauri kutekeleza majukumu yao.

Aidha, Kifungu cha 19 kinaeleza kuwa mtu anayekiuka masharti ya Sheria Ndogo hizo, pale ambapo hakuna adhabu maalum iliyowekwa, anaweza kutozwa faini isiyopungua Sh 200,000 na isiyozidi Sh milioni moja, au kifungo kisichopungua miezi 12 na kisichozidi miezi 24, au adhabu zote mbili.

Kwa msingi huo, Chalamila amesema kuanzia Jumatatu, Agosti 17, 2026, serikali itaanza kuchukua hatua dhidi ya mabasi yatakayoendelea kutumia vituo visivyo na vibali, huku akiahidi pia kuweka wazi majina ya kampuni sita zilizopewa vibali maalum.

Amesema vibali hivyo vitakapomalizika havitaruhusiwa kuhuishwa, hatua ambayo inalenga kuhakikisha mabasi yote ya mikoani yanaanza na kumalizia safari katika Stendi ya Magufuli.

Hatua hiyo, kwa mujibu wa Chalamila, inalenga kuweka mfumo mmoja unaoratibu usafiri wa mabasi ya mikoani na usafiri wa ndani ya jiji, kupunguza msongamano katika barabara za katikati ya Dar es Salaam na kuhakikisha miundombinu iliyowekezwa na Serikali inatumika kwa ufanisi, huku shughuli za usafirishaji zikifanyika kwa kuzingatia utaratibu na masharti ya kisheria yaliyowekwa na Halmashauri.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...