Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MWAMKO WA ULIPAJI KODI KWA HIARI, CHACHU YA MWELEKEO WA KUJITEGEMEA KIBAJETI KWA ASILIMIA 74.2


 NA: DK. REUBENI LUMBAGALA

Waasisi wa taifa letu walipambana na wakoloni ili kujinasua kutoka kwenye makucha ya kutawaliwa na kuamuliwa nini cha kufanya ili hali uwezo wa kufanya hivyo tulikuwa nao.

Disemba 09, 1961, tukapata uhuru kamili wa kisiasa lakini tukiwa hoi kiuchumi, hivyo kuwa na wajibu wa kujenga uchumi imara wa kutufanyia tuheshimike kwa wengine.

Wenye wajibu wa kujenga uchumi ni wananchi wenyewe wa nchi husika. Mathalani, kwa Tanzania, ni sisi Watanzania wenyewe ambao tunawajibika kuijenga nchi yetu kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Ni hivi: Hatuna mjomba wala shangazi wa kuja kuijenga Tanzania yetu. Ni sisi Watanzania wenyewe ndiyo wahusika wa kuijenga nchi yetu, kuhakikisha tunatatua changamoto zilizopo na kukuza ustawi wetu kwa maendeleo endelevu.

Kazi kubwa ya kujenga uchumi imara na uboreshaji wa huduma za kijamii, inategemea sana uwepo wa raslimali fedha za kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Swali linakuja, tunapata wapi fedha za kutekeleza miradi na mipango ya maendeleo? Majibu yanaweza kuwa mengi, lakini jibu la msingi ni kupitia ukusanyaji wa kodi kutoka kwa wananchi wenyewe.

UMUHIMU WA TRA KATIKA KUFANIKISHA MIPANGO YA MAENDELEO

Julai 1, 1996, serikali ikaanzisha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambapo hadi kufikia Julai 1, 2026, Mamlaka hiyo imetimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake. 

Pamoja na majukumu mengi ya TRA, moja kubwa ni kukusanya kodi kutoka kwa wadau kama vile wafanyabiashara, wafanyakazi, wajasiriamali, wawekezaji na wananchi kwa ujumla wenye sifa za kulipa kodi.

Kwa hakika, mageuzi makubwa yaliyofanywa, imeiwezesha TRA kuongeza mapato kutoka shilingi bilioni 531 mwaka wa fedha 1996/1997 hadi trilioni 32 mwaka 2025/2026.

Maono ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni kuifanya Tanzania kujitegemea kwa asilimia kubwa badala ya kutegemea misaada na mikopo ya wahisani, ambayo wakati mwingine imejaa masharti magumu, kutunyima uhuru wetu na hata kutweza utu wetu.

Aidha, kutokana na maono hayo, mapema mwezi Aprili 2021, Rais Dk. Samia alitoa maelekezo mahsusi kwa TRA kuongeza makusanyo ya kodi lakini kodi hizo zisiwe za dhulma, uonevu, ubabe na mabavu.

Ukweli ni kuwa, Rais alikuwa tayari mapato ya nchi yashuke hata kwa miezi miwili au mitatu, lakini kujengwe misingi imara na rafiki katika ukusanyaji kodi bila kuwaumiza walipakodi na wananchi ambao ndiyo nyenzo ya ujenzi wa taifa.

Leo, TRA inapoadhimisha miaka 30 na taifa letu linaloelekea maadhimisho ya miaka 65 ya uhuru wake, tuna kila sababu ya kusema "Tumeupiga mwingi katika makusanyo ya kodi, lakini tusibweteke, tuna kazi kubwa ya kujenga taifa linalojitegemea".

Nasema haya kwa sababu, bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027, asilimia 74.2 ni mapato ya ndani. Ni matunda ya Watanzania kusema tunaweza tutajenga nchi kwa nguvu zetu, kama kusaidiwa basi tusaidiwe katikati ya safari ya ujenzi wa Taifa letu, tena tusaidiwe kwa heshima kwa kuzingatia Tanzania imeimarisha sana diplomasia hasa ya kiuchumi na mataifa mengi ulimwenguni.

Hivyo, niwapongeze walipakodi na wananchi ambao wameipa heshima nchi yetu kwa kuongeza makusanyo ya kodi kwa mafanikio makubwa. Mwelekeo wa kujitegemea kibajeti utafanikiwa zaidi ya tulivyo sasa endapo kila mwenye sifa ya kulipa kodi atatimiza wajibu wake wa kulipa kodi tena kwa hiari.

Julai 01, 2026, Rais Dk. Samia alihudhuria hafla ya Tuzo za Rais kwa Walipakodi katika Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam. Katika hafla hiyo, Rais alikemea "Kodi ya dhulma na dhulma ya kodi".

Alifafanua kuwa, kodi ya dhulma ni kumlipisha mlipakodi zaidi ya kiwango kinachopaswa kulipwa na dhulma ya kodi ni kulipa kiwango cha chini cha kile kinachopaswa kulipwa.






Kimsingi, msisitizo wa Rais ni kuwa, kila anayepaswa kulipa kodi alipe kiwango kinachopaswa kulipwa ili kujenga uchumi imara, shindani na jumuishi kwa maendeleo endelevu ya kizazi cha sasa na kijacho.

Maoni: 0620 800 462.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...