Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AHITIMISHA MAFUNZO YA CHUO CHA UKAMANDA NA UNADHIMU DULUTI



 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 27 Juni, 2026 amehitimisha rasmi mafunzo ya mwaka mmoja ya Kozi ya Ukamanda na Unadhimu katika Mahafali ya 40 ya Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Tanzania, yaliyofanyika katika chuo hicho kilichopo Duluti, mkoani Arusha.

Mahafali hayo, ambayo Dkt. Nyansaho alikuwa Mgeni Rasmi, yalihusisha jumla ya maafisa wahitimu 82 kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na maafisa kutoka nchi mbalimbali rafiki. Mbali na kuhitimu Kozi ya Ukamanda na Unadhimu, wahitimu hao pia walitunukiwa Shahada za Umahiri na Stashahada katika Masuala ya Ulinzi na Usalama, mafunzo yaliyotolewa sambamba na kozi hiyo ili kuwawezesha kupata maarifa ya kina kuhusu masuala ya ulinzi, usalama na uongozi wa kimkakati.

Akizungumza katika mahafali hayo, Waziri wa Ulinzi na JKT aliwapongeza wahitimu kwa mafanikio yao, akieleza kuwa kuhitimu kozi hiyo ni ushahidi wa bidii, nidhamu, ujasiri, uthabiti na kujitolea kwao katika kipindi chote cha mafunzo. Alibainisha kuwa kozi hiyo ni miongoni mwa mafunzo ya kijeshi yanayotambulika kimataifa na kwamba wahitimu wanapaswa kujivunia mafanikio hayo makubwa.

“Mmethibitisha uwezo wa kukabiliana na changamoto za mafunzo makali na mmeonesha sifa za uongozi zinazohitajika kwa viongozi wa kijeshi wa sasa na wa baadaye. Mafanikio haya ni hatua muhimu katika safari yenu ya uongozi na utumishi kwa mataifa yenu,” alisema Dkt. Nyansaho.

Aidha, Waziri huyo aliushukuru uongozi wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu chini ya Mkuu wa Chuo hicho, Meja Jenerali Stephen Mnkande, kwa maandalizi mazuri ya mafunzo hayo na kwa kumpa heshima ya kuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 40 ya chuo hicho.

Katika hotuba yake, Dkt. Nyansaho alisisitiza kuwa majeshi ya ulinzi yanaendelea kuwa alama ya umoja wa kitaifa, uhuru na mshikamano wa mataifa. Alieleza kuwa pamoja na jukumu la msingi la kulinda mipaka na mamlaka ya nchi, majeshi ya ulinzi yameendelea kutoa mchango mkubwa katika kukabiliana na maafa, kujenga miundombinu, kushiriki katika shughuli za maendeleo ya taifa pamoja na kushiriki katika operesheni za kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa na taasisi mbalimbali za kikanda.

Waziri huyo pia alieleza kuwa mazingira ya usalama duniani yanaendelea kubadilika kwa kasi na kuibua changamoto mpya na ngumu zaidi za kiusalama, zikiwemo vita vya kisasa, ugaidi, uhalifu wa kimtandao, mashambulizi ya kiteknolojia na vitisho vingine vya kiusalama vinavyovuka mipaka ya nchi. Alisisitiza kuwa hali hiyo inahitaji majeshi ya ulinzi kuendelea kujiimarisha, kubadilika na kuendana na mahitaji ya wakati.

“Dunia ya leo inakabiliwa na mazingira mapya ya kiusalama ambayo yanahitaji viongozi wenye uwezo wa kufikiri kimkakati, kufanya maamuzi sahihi kwa wakati na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zisizotabirika. Elimu mliyoipata imewaandaa kwa jukumu hilo kubwa,” alisisitiza.

Kwa upande wa maafisa wanawake waliohitimu, Dkt. Nyansaho aliwapongeza kwa mafanikio yao na kueleza kuwa ushiriki wao katika kozi hiyo ni ushahidi wa maendeleo makubwa yaliyofikiwa katika kuhakikisha ushiriki wa wanawake katika sekta ya ulinzi na usalama unaimarishwa.

Alisema kuwa wanawake ni sehemu muhimu ya jumuiya ya kijeshi na kwamba kuhitimu kwao kunathibitisha kuwa wanawake wana uwezo wa kutekeleza majukumu ya ulinzi na usalama kwa ufanisi, weledi na kujituma bila kujali tofauti za kijinsia.

Aidha, alieleza kuwa Tanzania inajivunia kuongozwa na Rais wa kwanza mwanamke, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama. Kwa mujibu wa Waziri huyo, uongozi wake ni ushahidi wa uwezo wa wanawake kushika nafasi za juu za uongozi na mchango wao katika kuimarisha amani, usalama na maendeleo ya taifa.

Aidha Dkt. Nyansaho akaongeza kwa kuwaambia wahitimu hao, “Natambua mmepewa dhamana kubwa ya uongozi, mawazo ya kimkakati na ustadi wa kufanya maamuzi. Nyinyi ni viongozi wa baadaye wa majeshi yetu, walinzi wa usalama wa mataifa yetu na walinzi wa uhuru wetu unaothaminiwa.”

Aliongeza kuwa elimu na ujuzi walioupata utakuwa msingi imara wa utekelezaji wa majukumu yao ya baadaye na utawasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali watakazokutana nazo katika utumishi wao.

Waziri huyo pia aliwakumbusha wahitimu kuwa uongozi wa kweli hauhusu vyeo au nyadhifa, bali unahusu uwezo wa kuongoza kwa mfano, kuhamasisha wengine, kufanya kazi kwa ushirikiano na kudumisha maadili ya heshima, uadilifu, nidhamu na uwajibikaji.

“Ulimwengu tunaouishi unabadilika kila siku na changamoto za kiusalama zinazidi kuwa ngumu na zisizotabirika. Mnapaswa kutumia maarifa na uwezo mliopewa kukabiliana na changamoto hizo kwa ujasiri, ubunifu na uthabiti,” alisisitiza.

Vilevile, Waziri wa Ulinzi na JKT alizishukuru nchi rafiki za Burundi, Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Misri, Ethiopia, Kenya, Eswatini, Malawi, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Uganda, Zambia na Zimbabwe kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja za mafunzo ya kijeshi kwa kutuma maafisa wao kushiriki katika Kozi ya Ukamanda na Unadhimu.

Alieleza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inathamini ushirikiano na urafiki wa muda mrefu uliopo kati yake na mataifa hayo, na kwamba ushirikiano huo utaendelea kuimarishwa kupitia mafunzo ya pamoja, kubadilishana uzoefu na ushirikiano katika masuala ya ulinzi na usalama.

Mahafali hayo ya 40 ya Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Duluti yalihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Wakuu wa Majeshi wastaafu wa JWTZ, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Luteni Jenerali Salum Haji Othman, Wakuu wa Kamandi za JWTZ, Wakuu wa Vyuo vya Ukamanda na Unadhimu vya Afrika Mashariki, Wakuu wa Vyuo vya Kijeshi vya JWTZ, Waambata wa Kijeshi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania, maafisa wakuu kutoka Makao Makuu ya JWTZ pamoja na makamanda wa vikosi mbalimbali vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.


















Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...