Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MBUNGE AGNES ATOA ELIMU KWA WASAFIRISHAJI KUHUSU MIKOPO YA BODABODA NA BAJAJI


Na Ghati Msamba, Musoma.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Agnes, ametoa elimu kwa wasafirishaji wa bodaboda na bajaji kuhusu fursa za mikopo inayolenga kuwawezesha kupata vitendea kazi na kujikwamua kiuchumi, huku akiwataka kutumia fursa hizo kwa uaminifu na kurejesha mikopo kwa wakati.

Akizungumza katika mkutano na wasafirishaji hao, Mbunge Agnes alisema mikopo hiyo ni miongoni mwa fursa zinazolenga kuwawezesha vijana kuongeza kipato, kuboresha maisha yao na kutoka katika kiwango cha chini cha kiuchumi kwenda kwenye kiwango cha kati.

Alisema vijana hao wana nafasi ya kunufaika na mabilioni ya fedha yanayotolewa kupitia programu mbalimbali za kuwawezesha kiuchumi, ikiwemo kupata bodaboda na bajaji zitakazowawezesha kujiajiri na kuongeza kipato.

Mbunge huyo alisema anajivunia kuwa sehemu ya jitihada za kuwawezesha vijana, akieleza kuwa ana faraja kubwa kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi za kuinua wananchi kiuchumi.

“Rais Samia amefanya mambo mengi katika kuwawezesha wananchi. Mimi mwenyewe ni mmoja wa watu ambao nimepata faraja kutokana na fursa zilizopo, kwani zamani nilikuwa muuza dagaa. Leo nimepata nafasi ya kuwa mbunge na ninapaswa kutumia nafasi hii kuwahudumia wananchi,” alisema.

Aidha, aliwataka wanufaika wa mikopo hiyo kuwa waaminifu kwa kuhakikisha wanarejesha fedha walizokopa kwa wakati, ili kuwapa nafasi wananchi wengine kupata mikopo hiyo na wao wenyewe kuweza kukopa tena pale wanapohitaji.

Alisema urejeshaji wa mikopo ni muhimu kwa sababu fedha hizo zinapozunguka huwezesha watu wengi zaidi kunufaika na programu hizo.

Mbunge Agnes pia aliwataka wasafirishaji hao kutosikiliza taarifa za upotoshaji kutoka kwa baadhi ya watu wanaowashauri kutorejesha mikopo kwa madai kwamba mikopo hiyo ni sehemu ya siasa.

“Msidanganywe na watu wanaowaambia msirejeshe mikopo kwa sababu eti ni siasa. Mkopo ni wajibu na unapaswa kurejeshwa ili wengine nao wapate fursa. Tukitumia vizuri fursa hizi, tunaweza kubadilisha maisha yetu,” alisema.

Kwa upande mwingine, Mbunge Agnes alisema amebaini kuwa baadhi ya wasafirishaji katika eneo hilo wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vitendea kazi, hali inayowafanya washindwe kuongeza kipato na kuboresha maisha yao.

Alisema lengo la kuwafikishia elimu kuhusu mikopo hiyo ni kuhakikisha wanapata uelewa sahihi wa taratibu, masharti na namna bora ya kutumia mikopo hiyo katika shughuli za uzalishaji.

Akizungumzia kauli za baadhi ya watu wanaodai kuwa anatumia shughuli hizo kufanya kampeni, Mbunge Agnes alisema yeye ni mwakilishi wa wananchi aliyechaguliwa na ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Ilani ya Chama chake.

“Tuache propaganda za watu wanaosema Agnes anafanya kampeni. Mimi ni mbunge niliyechaguliwa na wananchi, hasa akina mama, na ninafanya kazi niliyotumwa. Nataka niache alama katika kuwahudumia wananchi,” alisema.

Aliongeza kuwa viongozi wanapaswa kuwatumikia wananchi kwa vitendo kwa kuwa wananchi ndio waliowapa dhamana ya kuwaongoza.

“Tunapaswa tuwahudumie wananchi kwa sababu mlituchagua ili tuwahudumie. Mimi sihitaji maneno mengi, ninachotaka ni kuona wananchi wanapata huduma na fursa zinazoweza kubadilisha maisha yao,” alisema.

Kwa upande wake, Afisa Mikopo kutoka Benki ya CRDB, Samwel, aliwataka wasafirishaji hao kutumia vizuri fursa hiyo ya mikopo na kuhakikisha wanatimiza masharti yaliyowekwa, ikiwemo kurejesha mikopo kwa wakati.

Samwel pia alimpongeza Mbunge Agnes kwa kuwashirikisha wananchi katika fursa hizo, akisema wapo baadhi ya watu wanaopata fursa za kiuchumi lakini hawako tayari kuwashirikisha wengine.

“Tunapaswa kumshukuru Mbunge Agnes kwa sababu kuna watu wengine wanapata fursa kama hizi lakini wanakuwa wagumu kuwashirikisha wananchi. Anapopatikana mtu anayewafikishia wananchi fursa na elimu kama hii, anapaswa kupewa pongezi,” alisema.

Aliwataka wasafirishaji hao kuchangamkia fursa hiyo kwa kuzingatia masharti ya mikopo na kutumia fedha kwa malengo yaliyokusudiwa, ili waweze kukuza shughuli zao za usafirishaji na kuongeza kipato.

Mkutano huo umeelezwa kuwa sehemu ya jitihada za kuwafikishia vijana taarifa kuhusu fursa za uwezeshaji kiuchumi, hususan mikopo inayoweza kuwasaidia kupata vitendea kazi na kujenga uwezo wa kujitegemea kupitia shughuli za usafirishaji. 









Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...