Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WMA: VIPIMO VISIVYO SAHIHI FAINI HADI MILIONI 100

 Kutokana na baadhi ya wafanyabiashara nchini kutumia vipimo visivyo sahihi katika kuwahudumia wananchi, Wakala wa Vipimo Nchini (WMA) umewaonya wafanyabiashara wanaotumia vipimo visivyokidhi viwango kuwa wanakabiliwa na adhabu kali kwa mujibu wa sheria, ikiwemo faini na kifungo. Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 18, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO, Mtumba jijini Dodoma, Afisa Mtendaji Mkuu wa wakala wa vipimo nchini (WMA), Alban Kihulla, amesema mtuhumiwa anayekubali kosa anaweza kutozwa faini ya Shilingi 100,000 hadi milioni 20 kwa kosa moja. Amesema kwa anayekataa kosa na kupatikana na hatia mahakamani, adhabu ni faini ya Shilingi 300,000 hadi milioni 50, au faini pamoja na kifungo kisichozidi miaka miwili. Kwa mkosaji wa mara kwa mara, amesema faini inaweza kufikia Shilingi milioni 100 kwa kosa moja, hatua inayolenga kuhakikisha wafanyabiashara wanatumia vipimo sahihi na kulinda haki za walaji. Kihulla amewataka wafanyabiashara na wakulima kuachana ...

RC SAGINI AJITAMBULISHA RASMI CCM MBEYA, AWEKA MSISITIZO UTEKELEZAJI WA ILANI NA USHIRIKIANO KATIKA KUHARAKISHA MAENDELEO

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Jumanne Abdallah Sagini, amefanya ziara rasmi katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya zilizopo jijini Mbeya, ikiwa ni sehemu ya kujitambulisha rasmi kwa viongozi wa chama pamoja na kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu ya maendeleo ya Mkoa. Katika ziara hiyo iliyofanyika Septemba 18, 2026, Mhe. Sagini amekutana na viongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya, ambapo ameeleza umuhimu wa kuwepo kwa ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na chama katika kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Amesisitiza kuwa Serikali ya Mkoa wa Mbeya itaendelea kuhakikisha ahadi na maelekezo yaliyopo katika Ilani ya Uchaguzi yanatekelezwa kwa vitendo, huku maslahi na mahitaji ya wananchi yakiendelea kuwa sehemu ya msingi katika utekelezaji wa shughuli za Serikali.

AGNES MARWA ATOA MSAADA WA SARUJI, TANKI LA MAJI NA VIFAA VYA MICHEZO MUSOMA

 NA GHATI MSAMBA, MUSOMA Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Agnes Methew Marwa, ametoa msaada wa mifuko 20 ya saruji, tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 500 pamoja na vifaa vya michezo katika Shule ya Msingi Azimio iliyopo mjini Musoma. Msaada huo umetolewa katika viwanja vya shule hiyo wakati wa mahafali ya 68 ya wahitimu wa Darasa la Saba mwaka 2026, ambapo Agnes alikuwa mgeni rasmi. Akizungumza katika mahafali hayo, Agnes aliwahimiza wahitimu kutokata tamaa katika safari yao ya elimu, akisisitiza kuwa kuhitimu elimu ya msingi si mwisho wa masomo, bali ni hatua ya kuendelea na elimu ya juu zaidi. Alisema yuko tayari kuwasaidia wanafunzi watakaofanya vizuri na kuendelea na kidato cha kwanza kwa kuwapatia baadhi ya mahitaji ya shule kupitia taasisi yake ya Agnes Foundation. “Nawahimiza msikate tamaa. Kuhitimu shule ya msingi si mwisho wa elimu. Endeleeni kusoma kwa bidii na kuitangaza vizuri Shule ya Msingi Azimio,” alisema Agnes. Aidha, Agnes alieleza kuwa juhudi zinazo...

OCPD INAVYOWEKA MSINGI WA KISHERIA WA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050

Maendeleo ya Taifa hayaishii kwenye kuwa na sera nzuri, mipango mikubwa au dira yenye malengo makubwa lakini nyuma ya kila hatua ya maendeleo inayokusudiwa kutekelezwa, kuna msingi mmoja muhimu unaowezesha Serikali kuchukua hatua kwa uhalali, utaratibu na uwajibikaji. Dira inaweza kuonyesha Tanzania inayotakiwa kujengwa, sera inaweza kuelekeza namna ya kufikia malengo hayo na mipango ikaainisha hatua zinazopaswa kuchukuliwa. Hata hivyo, bila mfumo madhubuti wa sheria unaoenda na wakati malengo hayo yanaweza kubaki kwenye nyaraka badala ya kugeuka kuwa matokeo yanayoonekana katika maisha ya wananchi. Hapa ndipo nafasi ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) inapofanya kazi kubwa katika kufikia lengo hilo la serikali na jamii kwa ujumla. Kupitia maandalizi na uboreshaji wa sheria Ofisi hii inashiriki katika kuweka msingi wa kisheria unaosaidia Serikali kutekeleza sera, mipango na mikakati yake katika mazingira yanayobadilika kiuchumi, kijamii na kiteknolojia.  Wajibu wa OCPD kati...

KAMBI YA MADAKTARI BINGWA KUFANYIKA MKOANI ARUSHA

 …..Itafantika katika hospitali ya JKCI-ALMC kuanzia tarehe 21 Na Mwandishi Wetu, Arusha Hospitali ya JKCI–ALMC Arusha (Selian ya Mjini) imeandaa Kambi Maalum ya Matibabu ya Kibingwa itakayofanyika kuanzia Septemba 21 hadi 24, 2026, ikiwakutanisha madaktari bingwa na wabobezi kutoka Tanzania na India. Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dkt. Tatizo Waane, alisema jana kuwa kambi hiyo itawakutanisha wataalamu kutoka Apollo Hospitals–India, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) pamoja na madaktari bingwa wa JKCI–ALMC Arusha (Selian ya Mjini). Alisema kambi hiyo imelenga kuwafikishia wananchi huduma za kibingwa katika maeneo ya magonjwa ya mfumo wa fahamu, upasuaji wa ubongo na uti wa mgongo, magonjwa na upasuaji wa mfumo wa mkojo, pamoja na magonjwa, upasuaji wa mifupa, viungo na majeraha. “Tunatarajia kuona wagonjwa kati ya 100 hadi 200 kwa siku. Watapata nafasi ya kuonana na madaktari bingwa, kufanyiwa tathmini, kupata us...

TANZANIA'S SENIOR FEMALE MILITARY DIPLOMAT LEAVES LEGACY IN ZAMBIA

 By Prosper Makene, LUSAKA, Zambia Tanzania's senior female military diplomat, Colonel Bula Bulali, has concluded her four-year tour of duty in Zambia, leaving behind a legacy of strengthened defence ties and groundbreaking cooperation between the two historic allies. Col. Bulali, who has served as Tanzania's Defence Advisor accredited to the Republic of Zambia since 2022, officially bade farewell to Zambia's Ministry of Defence and its Services on Tuesday, 17th September 2026. According to a Press Statement issued by the Ministry of Defence, her tenure was marked by tangible achievements in defence diplomacy, military training, and joint cooperation. Reflecting on her service, Col. Bulali said Zambia and Tanzania had scored significant success in enhancing people-to-people ties and military collaboration. She singled out the signing of a landmark Memorandum of Understanding (MoU) between the Zambia National Service (ZNS) and Tanzania's Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) earl...