RAIS SAMIA AZINDUA TUME MAALUMU KUBAINI CHANZO NA WAHUSIKA WA GHASIA ZA WAKATI NA BAADA YA UCHAGUZI 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua Tume ya Rais ya Uchunguzi ya Wahusika wa Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria Katika Matukio ya Ghasia Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, ikiwa na jukumu la kuchunguza kwa kina chanzo cha matukio hayo, wahusika pamoja na waliowezesha kutokea kwake. Akizungumza leo Ijumaa Agosti 7, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Tume hiyo, Rais Samia amesema ameunda Tume hiyo kwa kuzingatia mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Tume ya Uchunguzi, Sura ya 32, ili kuwezesha uchunguzi wa kina kuhusu matukio ya ghasia na ukiukwaji wa sheria yaliyotokea. Amesema Tume hiyo itaongozwa na Jaji Shabani Ally Lila na itakuwa na jumla ya makamishna sita, ambapo mmoja anatoka Uganda na mwingine Namibia, hatua inayolenga kuongeza mtazamo mpana katika utekelezaji wa jukumu hilo. “Katika Tume hii tumeamua kuwashirikisha wenzetu kutoka nje ya Tanzania ili kupata maono mapana,” amesema Rais Samia. Rais Sami...