Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MKOPO WA BILLIONI 600 KUTOKA UMOJA WA ULAYA KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI SAFI MWANZA

Jiji la Mwanza limepiga hatua nyingine katika jitihada za kutatua changamoto ya muda mrefu ya upatikanaji wa maji baada ya kusainiwa kwa mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Shilingi bilioni 39 kwa ajili ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Chanzo cha Maji Butimba. Mkataba huo uliosainiwa jijini Mwanza baina ya Umoja wa Ulaya (EU) na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), ni sehemu ya uwekezaji mkubwa unaolenga kuongeza uzalishaji wa maji, kuimarisha miundombinu ya usambazaji na kuhakikisha wakazi wa Jiji la Mwanza wanapata huduma ya maji yenye uhakika. Kwa sasa, Jiji la Mwanza linategemea vyanzo viwili vikuu vya maji vya Butimba na Capri Point ambavyo kwa pamoja vina uwezo wa kuzalisha takribani lita za ujazo milioni 138 za maji kwa siku. Hata hivyo, mahitaji ya maji kwa wakazi wa jiji hilo yamefikia takribani lita za ujazo milioni 188 kwa siku, hali inayosababisha kuwepo kwa nakisi ya takribani lita za ujazo milioni 50 za maji kila siku. Utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mr...

MWANZA WATER CRISIS: TSH600 BILLION PROJECT SET TO INCREASE SUPPLY CAPACITY

  The City of Mwanza has taken another major step towards addressing its long-standing water supply challenges after a concessional loan agreement worth TSh39 billion was signed to support the implementation of the Second Phase of the Butimba Water Source Project. The agreement, signed in Mwanza between the European Union (EU) and the French Development Agency (AFD), is part of a major investment aimed at increasing water production capacity, strengthening distribution infrastructure and ensuring reliable water services for residents of Mwanza. Currently, Mwanza City depends on two major water sources, Butimba and Capri Point, which together produce approximately 138 million cubic litres of water per day. However, the city’s water demand has increased to approximately 188 million cubic litres per day, leaving a deficit of about 50 million cubic litres daily. The implementation of the Second Phase of the Butimba Water Source Project is expected to significantly reduce this gap by in...

RAIS WA NAMIBIA KUFANYA ZIARA YA KITAIFA NCHINI

 Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mheshimiwa Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah, anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 19 Juni, 2026 kwa ziara ya kitaifa. Ziara hiyo, ambayo ni ya pili kuifanya nchini Tanzania tangu aingie madarakani, inaendelea kudhihirisha uhusiano wa kindugu na wa kihistoria kati ya Tanzania na Namibia, uliojengwa katika misingi ya harakati za ukombozi wa Afrika, mshikamano na ushirikiano wa maendeleo unaonufaisha wananchi wa pande zote mbili. Tarehe 20 Juni, 2026, Rais Nandi-Ndaitwah atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam, yatakayojikita katika masuala mbalimbali ya ushirikiano wa pande mbili pamoja na masuala ya kikanda na kimataifa katika maeneo yenye maslahi ya pamoja. Baadaye, viongozi hao wawili watazungumza na waandishi wa habari. Akiwa nchini, Rais Nandi-Ndaitwah atatembelea eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam, ambako aliwahi kuishi katika miaka ya...

TVLA YAWATAKA WAFUGAJI KUONGEZA MWITIKIO WA CHANJO ZA MIFUGO

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi, amewataka wafugaji nchini kuongeza mwitikio wa kuchanja mifugo dhidi ya magonjwa mbalimbali ili kuimarisha afya ya mifugo, kuongeza uzalishaji na kupunguza hatari ya maambukizi ya magonjwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Dkt. Bitanyi ametoa wito huo leo, Juni 18, 2026, mjini Morogoro wakati wa kikao cha pamoja kati ya TVLA na timu ya Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) unaotekelezwa chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Kikao hicho kililenga kujadili maeneo ya ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo. Amesema bado kuna mwitikio mdogo wa wafugaji wadogo katika kuchanja mifugo yao licha ya uwepo wa chanjo zinazozalishwa na TVLA, huku wafugaji wakubwa wakionesha ushiriki mkubwa zaidi katika kampeni za chanjo. “Tunaona mwitikio mkubwa zaidi miongoni mwa wafugaji wakubwa, lakini kwa wafugaji wadogo bado ni mdogo. Tunao utaalamu na wataalamu. Kupitia mradi huo,...

OFISI YA WAZIRI MKUU YATHIBITISHA NYENZO MUHIMU ZA KUIMARISHA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

 Na Mwandishi Wetu, Dodoma SERIKALI imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa nchini ili kuongeza uwezo wa kuzuia, kujiandaa, kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa, kufuatia kuongezeka kwa matukio yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi pamoja na vihatarishi vingine vya asili na kijamii. Hayo yameelezwa leo Juni 18, 2026 jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, wakati akifungua Kikao cha Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa kilicholenga kupitia na kuthibitisha Mwongozo wa Urejeshaji Hali Baada ya Maafa, Mwongozo wa Uendeshaji na Uratibu wa Uhawilishaji Fedha kwa Walioathirika wa Maafa, pamoja na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Maafa (DMIS). Brigedia Jenerali Ndagala amesema kuwa katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekumbwa na matukio mbalimbali ya maafa yakiwemo mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, u...

RAIS DKT. MWINYI: TANZANIA ITAENDELEA KULINDA MAZINGIRA YA BAHARI NA KUENDELEZA UCHUMI WA BULUU

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya za kimataifa katika kulinda mazingira ya bahari, kuimarisha usalama baharini na kuendeleza Uchumi wa Buluu wenye tija kwa wananchi. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema  hayo leo, tarehe 18 Juni 2026, jijini Mombasa, Kenya, wakati wa hafla ya kufunga Mkutano wa 11 wa Masuala ya Bahari (Our Ocean Conference), ambapo alimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Amesema mkutano huo umeimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kukabiliana na changamoto za bahari, huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza uwekezaji, teknolojia na ujenzi wa uwezo wa taasisi ili kutumia kikamilifu fursa za Uchumi wa Buluu kwa maendeleo endelevu. Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Serikali ya Kenya kwa kufanikisha mkutano huo na kusisitiza dhamira ya Tanzania ya kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kulinda bahari na kuendelez...