Na: Dawati la Habari Polisi Mwanza Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza (MPC) kimeshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Kuzuia Kuzama Maji Duniani, ambayo kimkoa yamefanyika katika Ufukwe wa Bismarck Rock, Capri Point jijini humo. Akizungumza kwenye maadhimisho hayo, Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Polisi Wanamaji Mwanza, SSP Abduhaj Mkombe kwa niaba ya Mkuu wa Chuo, amesema chuo hicho ni mdau mkuu katika kuhakikisha kinapunguza vifo vitokanavyo na ajali za majini katika Ziwa Victoria na maeneo mengine nchini. "Sisi kama Polisi tuna dhamana ya kusimamia usalama majini na kuhakikisha raia na mali zao wanakuwa salama. Tumeona ipo haja ya kushiriki kwenye tukio hili ili kuonyesha mchango wetu katika kupunguza vifo vinavyotokana na kuzama maji," amesema Mkombe. Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Christopher Ngubiagai, amelipongeza Jeshi la Polisi pamoja na vyombo vingine vya usalama kwa kufanya kazi kwa ushirik...
Marato tv - Sauti ya Jamii